• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WILAYA YA MASWA YAADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU KWA KUPANDA MITI

Posted on: December 9th, 2024

Wananchi wa Wilaya ya Maswa leo tarehe 09 Desemba 2024  wameadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara kwa kupanda miti katika maeneo mbalimbali ya taasisi za umma ambapo kiwilaya maadhimisho hayo yamefanyika  katika shule mpya ya sekondari inayojegwa katika Kijiji cha Isageng’he Kata ya Sukuma  ambapo zaidi ya miti mia tatu  imepandwa na Watumishi  pamoja na Wananchi wa kijiji hicho.

 Akizungumza na wananchi baada ya zoezi la upandaji wa miti Mkuu wa wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amewashukuru wananchi wa kijiji cha Isageng’he kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la upandaji wa miti lililofanyika katika eneo ambalo shule mpya ya sekondari inajengwa,  ambapo serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 584.

Aidha Mkuu wa Wilaya amewapongeza viongozi mbalimbali kutoka Halmashauri, Watumishi na Kamati ya Ulinzi na Usalama kwa kuitikia wito wa maelekezo ya serikali ambayo Mhe Rais alitoa  maelekezo kwa viongozi  kupanda miti, kufanya usafi katika maeneo ya taasisi mbalimbali za serikali.

Mhe Kaminyoge amesema Dkt Samia Suluhu Hassan ni championi wa mabadiliko ya tabia nchi kwa kuendelea kugawa majiko ya nishati safi ambayo itasaidia wananchi  kuepukana na matumizi ya kuni na mkaa ili miti inayopandwa iendelee kutunzwa kwa ajili ya vizazi na vizazi.

Pia Mkuu wa Wilaya  ametoa wito kwa wananchi wa Maswa kurudisha uoto wa asili ambao ulikuwepo enzi za mababu kwa kuwa miti inayopandwa ndio chanzo cha mvua.

“Tukipanda miti kama hivi majumbani, kwenye taasisi tunaongeza uwezekano wa kupunguza mabadiliko ya tabianchi sisi kama wananchi, mmoja mmoja nyumbani, vikundi tunahitaji kupanda miti”

Aidha Mhe Kaminyoge ametoa maagizo kwa viongozi na wananchi  wa kijiji hicho  kuhakikisha wanakuwa walinzi wazuri wa eneo lililopandwa miti ili mifugo isiharibu miti iliyopandwa na baada ya miaka mitatu faida ya miti hiyo ipatikane.

Sambamba na hilo pia amewataka wakala wa Huduma za  Misitu Tanzania (TFS ) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha kuwa miti milioni moja na laki mbili  iliyobaki igawiwe kwa wananchi pamoja na taasisisi ili lengo la wilaya kufikia miti milioni moja na laki tano likamilike

Kwa upande wake Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Duttu Lubinza amesema kuwa mikakati ya halmashauri ni kupanda miti milioni moja na laki tano ambapo mpaka sasa tayari miti zaidi ya laki tatu imepandwa katika taasisi za umma na watu binafsi.

Aidha ameongeza kuwa ili kufanikisha zoezi hilo Halmashauri kwa kushirikana na wakala wa misitu Tanzania  tayari imeweka vitalu katika shule za msingi na sekondari ambavyo vimebeba miche milioni moja na laki tano ili ifikapo januari 2025 miti hiyo ipandwe  na ugawaji wa miti unafanyika bure kwa wananchi ili waone umuhimu wa kuhifadhi misitu.

Kwa upande wake Saimoni Japhet amemshukuru Mhe  DC Kaminyoge kwa kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru katika kijiji hicho kwa  kupanda miti  ambapo wameahidi kusimamia kikamilifu ili wananchi wasiingize mifugo yao katika eneo hilo ambalo limepandwa miti na kuwataka wanachi  wenzake wakawe mabalozi katika kusimamia eneo hilo.

PICHA MBALIMBALI ZA MATUKIO 



Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.