• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Maendeleo ya Jamii

Idara ya maendeleo ya Jamii ina vitengo vitano ambavyo ni :

i.Kitengo cha utafiti takwimu na mipango.

ii.Kitengo cha wanawake na watoto

iii.Kitengo cha kikosi cha ujenzi

iv.Kitengo cha kudhibiti Ukimwi

v.Kitengo cha vijana

Kitengo cha utafiti takwimu na mipango

Shughuli zinazofanyika ni;

a.Uhamasishaji wa shughuli za kujitegemea ambazo ni pamoja na;

-Ujenzi wa madarasa, Zahanati, Vituo vya afya, na nyumba za walimu

-kushiriki katika utengenezaji wa barabara na uchimbaji wa visima.  

b.Ukusanyaji wa takwimu mbalimbali, mfano;

-Takwimu za watu wenye ulemavu

-Takwimu za vikundi

-Takwimu za ujenzi wa nyumba bora

-Takwimu za watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

-Takwimu za vituo vya kulelea watoto wadogo mchana

-Takwimu za wazee

c.Kusaidia vikundi kuandika maandiko ya miradi

d.Kusaidia kuelekeza jamii katika upangaji mipango ya maendeleo.

e.Kuwezesha jamii kutambua matatizo waliyonayo na hivyo kuyapanga kulingana na umuhimu wake kisha kuyatatua kwa kutumia fursa na rasmali walizonazo.

f.Kutafsiri  na kusimamia utekelezaji wa sera za Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto.

g.Kusimamia utafiti kuhusu matatizo mbalimbali katika jamii.

h.Kutambua azaki zilizomo katika wilaya na kuratibu shughuli zake.

Kitengo cha wanawake na watoto

Shughuli zinazofanyika ni;

i.Utoaji wa elimu ya ujasiliamali kwa vikundi vya wanawake.

ii.Kuelimisha jamii juu ya athari ya mila na desturi potofu zinazogandamiza wanawake na watoto.

iii.Kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana.

iv.Kutembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

v.Kufanya ufuatiliaji na  kutoa ushauri kwa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana.

vi.Kuelimisha jamii katika masuala mazima ya usawa wa kijinsia.

vii.Uundaji wa vikundi vya wanawake vya kiuchumi.

viii.Kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake.

ix.Kutoa vifaa vya michezo na vya  kujifunzia kwa watoto wa chekechea

Kitengo cha vijana

Kitengo cha vijana  kinafanya kazi zifuatazo;

a.Utoaji wa elimu ya ujasiliamali kwa vikundi vya vijana.

b.Kuelimisha vijana  juu ya umuhimu wa kuunda vikundi na kufanya kazi zao katika vikundi

c.Kufanya ufuatiliaji na  kutoa ushauri kwa vikundi vya vijana

d.Uundaji wa vikundi vya vijana vya  vya kiuchumi  

e.Kutoa mikopo kwa vijana.kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini.

f.Kutoa vifaa / baiskeli kwa watu wenye

Kitengo kikosi cha ujenzi

Shughuli zinazofanyika

i.Kuhamasisha vijana kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali kupitia fani za ufundi kama vile ufundi Mwashi, Uselemala , uhunzi na uchomeleaji.

ii.Kutoa mafunzo kwa vikundi vya mafundi kwa kushirikiana na taasisi zingine za serikali kama vile mamlaka ya ufundi stadi VETA.

iii.Kuibua na kusambaza teknolojia rahisi na sahihi zinazoweza  kuisaidia jamii katika shughuli za kila siku kwa lengo la kujiletea maendeleo.

iv.Kushirikiana na kamati za miradi ya maendeleo kwenye ngazi ya kata na vijiji katika kusimamia shughuli za miradi ya maendeleo zinazotekelezwa na jamii.

v.Kutoa tafsiri ya teknolojia mpya juu ya matumizi yake mfano ujenzi wa nyumba bora na zenye gharama nafuu kwa kutumia matofari yanayotengenezwa kwa kutumia mashine za Cinvarumm Interlocking pamoja na Hydroform mashine.

vi.Kuhamasisha jamii ili iweze kujijengea makazi bora kwa maana ya nyumba za kuishi ikiwa ni pamoja na kutoa tafsiri ya nyumba bora kwa kutaja sifa zake ambazo ni ; nyumba bora imejengwa kwa kuzingatia sifa za majenzi , msingi uliojengwa kwa mawe au matofari , ukuta imara , madirisha yanayoingiza mwanga na hewa ya kutosha ndani, iliyo na jiko na choo pamoja na store sambamba na hayo lazima iwe na shimo la kutupia taka ngumu na laini.

vii.Kusimamia shughuli za miradi ya maendeleo zinazotekelezwa kwa kutumia nguvu za wananchi mfano ujenzi wa vyumba vya madarasa , vyoo na zahanati.

viii.Kutoa mwelekeo kwa vikundi vya ujasiliamali kuona kwamba uwezekano wa kujiletea maendeleo katika maeneo yao inawezekana kwa kutumia raslimali walizonazo kwenye maeneo yao na wataalamu waliopo.

Kitengo cha kudhibiti UKIMWI

Kitengo hiki kinajishughulisha na udhibiti wa V.V.U na UKIMWI. Lengo kuu ni kuboresha huduma za V.V.U na UKIMWI kuhamasisha na kuelimisha jamii kujikinga na  maambukizi mapya  ya V.V.U. Ili kufanikisha lengo ,  Wilaya haina budi  kuungana na  Serikali kuu kuunganisha nguvu za Serikali za Mitaa, Mashirika yasiyo ya Kiserikali na vikundi vya kijamii vikiwepo vya Watu wanaoishi na Virusi Vya UKIMWI kushughulikia Afua ( Intervention)  zifuatazo;

-Mazingira wezeshi

-Kinga

-Matunzo na matibabu

-Kupunguza athari za V.V.U na UKIMWI kwa jamii

Huduma za kijamii

i.Pamoja na shughuli zinazoratibiwa na Idara kupitia vitengo vyake pia  huratibu shughuli na huduma za jamii kama ifuatavyo; Huduma za ibada katika madhehebu ya  Kiislam, Katoliki,AEGT,FB Fellowship,

CALVARY,The Pool of Sloam, SABATO, AIC, FPCT, ANGLICAN, KKKT, PAG,TDG, OMEGA, KLAPT, MALAMPAKA na SAYUNI.

ii.Biashara mbalimbali  kama vile biashara za mazao ya kilimo cha pamba, alizeti, mahindi, mpunga,viazi vitamu, choroko, kunde, dengu, karanga, njugu mawe, ufuta,  mboga mboga na matunnda.

iii.Shughuli za ufugaji  wa Ng’ombe, mbuzi, kondoo,nguruwe,nyuki,kuku, na bata.

iv.Shughuli za minada, magulio  na masoko .

v.Kumbi za mikutano za  Halmashauri ya wilaya , Ndemax na Millenium.

vi.Huduma za Mahakama 13 na magereza 2.

vii.Shughuli katika shule za  awali 120, kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi (Dekapori), chuo cha maendeleo ya wananchi , kituo cha kulelea watoto wenye mtindio wa   ubongo (Binza Primary), na jengo la shughuli za wananchi (SIDO).

viii.Huduma za kifedha katika taasisi za NMB, CRDB, POSTA, BAYPOT, VISION FUND na PRIDE.

ix.Huduma za mawasiliano katika taasisi za TTCL, AIRTEL, VODACOM, TIGO, ZANTEL,HALOTEL TANESCO NA REDIO SIBUKA


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.