• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC Anney, azindua chanjo ya Mifugo wilayani Maswa

Posted on: August 30th, 2025

Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Mkoa  wa  Simiyu  imezindua  chanjo  ya  Mifugo  kwa  ajili  ya  kukinga  mifugo  dhidi  ya  magonjwa  mbalimbali ikiwemo homa ya mapafu kwa Ng’ombe. Mifugo inayotarajiwa kuchanjwa ni Ng’ombe, Mbuzi, Kondoo na Kuku.

Akizindua  zoezi  la  chanjo  hiyo, Mkuu  wa  wilaya  ya  Maswa  Mhe  Dkt  Vicent  Naano  Anney amesema  lazima  zoezi hili  linasimamiwe  vyema  ili  mifugo yote  ichanjwe  kwani  ni  lazima  wala siyo  hiari. 

Akisisitiza alisema “Zoezi la chanjo ya Mifugo siyo la hiari ni lazima maana lipo kisheria na linasaidia kupunguza magonjwa ya mlipo kwa mifugo hivyo Wafugaji wote muone umuhimu wa zoezi hili kwakuwapeleka mifugo wenu wakapate chanjo”  Dc Maswa Dkt Vicent Anney 

Pia  amewashauri  wafugaji kutafuta  mbegu  bora  za  mifugo  ili kuleta  ushindani  katika  soko la  nyama  nje  ya  nchi na  kuongeza  uchumi na  tija  kwa  wafugaji  huku  akiagiza wataokaidi kuchanja  mifugo  yao  wapelekwe Mahakamani  kwa  hatua za  kisheria. 

 Naye Daktari  wa  Mifugo katika  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Dkt Charles  Msira ametaja idadi ya  mifugo  na malengo waliyojiwekea  katika  kufanikisha  zoezi  hilo  la  uchanjaji wa  mifugo. Aidha Dkt Msira amesema  kuwa  chanjo  hii  ni  Muhimu  kwa  mifugo  kwani  itaenda kudhibiti milipuko  ya  magonjwa  ya  mifugo, kuongeza  uzalishaji wa  mazao ya  mifugo yenye  Ubora  na  Salama  kwa  watumiaji  huku akitaja  hasara  za  kutochanja  mifugo.

Nao  baadhi  ya  wafugaji wa  Kata ya  Nyabubinza  wakaelezea  furaha  yao baada  ya  kuletewa huduma  ya  chanjo  katika eneo lao huku wakilinganisha hapo  awali  walikuwa  wanapoteza  mifugo  kutokana  na  magonjwa mbalimbali  na  kutumia  fedha  nyingi  kutibu mifugo  yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC Anney, azindua chanjo ya Mifugo wilayani Maswa

    August 30, 2025
  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.