• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

Posted on: August 6th, 2025

Shirika la Nutrition International kwa ushirikiano na World Vision - Tanzania chini ya uangalizi wa Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wamefanya uwasilishaji wa matokeo ya utafiti wa kutathmini hali ya jinsia, vijana balehe na lishe katika mkoa wa Simiyu. Utafiti huu ni sehemu ya mradi uitwao “Realizing Gender Equality, Attitudinal Change, Transformative Systems in Nutrition-(REACTS-IN)” unaotekelezwa katika wilaya za Maswa na Meatu, Mkoa wa Simiyu. Utafiti huu ulifanyika ili kupata taarifa zitakazotumika kuandaa utaratibu wa kupangilia mradi wa REACTS IN na kuhakikisha kuwa mradi huu unafikia malengo yake ya kuwainua vijana rika balehe walio katika mazingira magumu, ili kukidhi mahitaji yao muhimu ya usawa wa kijinsia na lishe. Uwasilishaji wa matokeo haya ya utafiti ulilenga kuwajulisha wadau wote muhimu wa mradi hali halisi ilivyo kuhusiana na hali ya usawa wa kijinsia na lishe miongoni mwa vijana balehe katika mkoa wa Simiyu ili kubaini na kupanga mikakati halisia itakayoweza kuboresha huduma za afya ya uzazi na lishe kwa vijana balehe.


Matokeo ya utafiti huo yameonyesha kwamba, vijana balehe wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma stahiki za lishe na afya ya uzazi na jinsia kutokana na mila na desturi, ndoa za mapema kwa wasichana na changamoto za mifumo ya kutolea huduma katika jamii. Hali kadhalika, ingawa Serikali imeweka mikakati mizuri na yenye tija kuwahudumia vijana balehe wa makundi yote, jamii kwa ujumla wake bado haijajipanga kiasi cha kutosha kuwahudumia vijana balehe wenye mahitaji maalumu katika maeneo mbalimbali kama vile mashuleni, katika vituo vya kutolea huduma za afya n.k.


Ushauri umetolewa kwa Serikali ya Mkoa na wadau wake kuishirikisha jamii katika kukuza uelewa wa masuala ya haki ya kijinsia, lishe na afya ya uzazi kwa vijana balehe ili kusaidia ukuaji wenye tija wa kundi hili maalumu la vijana kwa maisha yao ya sasa na baadaye.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.