• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

Posted on: June 10th, 2025

Walimu wa awali kutoka shule 135 za msingi Wilayani Maswa wamepatiwa mafunzo maalumu  ya mbinu bora za kufundisha  wanafunzi wa madarasa ya awali ili waweze kumudu stadi za  kusoma, kuandika na kuhesabu pamoja na kumudu madarasa makubwa. Mafunzo hayo yametolewa na progammu ya Shule Bora  katika ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana Maswa iliyopo Kata ya Sukuma Wilayani Maswa Mkoani Simiyu.

Afisa Elimu Taaluma ambaye pia ni Mratibu wa Shule Bora Wilaya ya Maswa Mwl. Neema Makundi alisema mafunzo waliyoyapata walimu hao yatawaongezea uwezo wa kumudu madarasa  kutengeneza zana mbalimbali ambazo zitawavutia wanafunzi na kuongeza maudhurio na kuwafanya watoto hao kusoma kwa urahisi.

Pia Mwl Makundi alitoa wito kwa walimu hao baada ya kupata mafunzo hayo wakalete mabadiliko katika shule zao kwa kupunguza idadi ya watoto wasiojua KKK na kuongeza maudhurio pamoja na upendo kwa  watoto katika madarasa yao.

Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Chuo cha Ualimu Bunda Mwl. John Ndimbo   alisema mbinu walizozipata walimu zitaenda kusaidia watoto kumudu stadi za KKK na kumudu madarasa makubwa.  

“Katika mafunzo haya watoto wamewezeshwa mbinu na moja ya mbinu hizo ni nyimbo, michezo na ngojera ambazo walimu wanaweza kuzitumia ili kulifanya darasa kuwa changamfu pamoja na kuwafikia  watoto  wote kulingana na mahitaji yao.” Alieleza Mwl. Ndimbo

Aidha aliwasisitiza kuwa serikali imetumia gharama kuandaa mafunzo hayo hivyo amewataka walimu hao mafunzo waliyoyapata waende wakayatekeleze kwa weredi ili kuweza kupunguza changamoto za watoto kumudu stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.

Kwa upande wake Mwalimu wa shule ya msingi Inenwa Mwl. Paul Julius alisema baada ya mafunzo hayo ufundishaji utarahisishwa kwa kuwa wamepata mbinu bora za kutengeneza dhana na kumudu ufundishaji wa madarasa makubwa ya wanafunzi.

Nae Mwl. Lilian Israel kutoka shule ya msingi Mwasayi alisema mafunzo hayo yamewasaidia kuboresha namna ya kufundisha watoto  kwa kutumia  mbinu na  dhana za kufundishia ambazo watoto wakiziona watafurahia na kuelewa kwa haraka kwa kuwa zitakuwa zinajieleza zenyewe.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.