• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Waziri Mkuu atembelea miradi ya maendeleo wilayani Maswa

Posted on: March 27th, 2023

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan ili kuona utekelezaji wa miradi hiyo ilipofikia.

Waziri Mkuu amezindua jengo la matibabu ya  dharura katika hospitali ya Wilaya ya Maswa iliyopo Kata ya Sola ambalo limejengwa kwa shilingi milioni mia tatu 300.

Mhe. Waziri Mkuu akizindua Jengo la  Matibabu ya Dharula katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa 26.03.2023

Mhe. Majaliwa alisisitita kuwa jengo  hilo la matibabu ya dharura  limejaa  vifaa vya kisasa  na linatoa huduma kwa wakazi wa  Maswa  na maeneo mengine kwa wagonjwa wote hasahasa kina mama wajawazito na madereva bodaboda waliopata ajali.

Mhe. Waziri Mkuu aliongeza kuwa wilaya ya Maswa ni wilaya ya kiuchumi na inasimamia na kuhamasisha maendeleo ya kiuchumi katika wilaya zingine hivyo jengo hilo la dharura linapaswa kuwepo ili kutoa huduma kwa wananchi wote wa Maswa na mikoa mingine kwa kuwa barabara zimetengenezwa na wananchi wengi wanapita hapo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa TAMISEMI Dkt Festo Dugange alisema uboreshaji wa sekta ya afya unaendelea ambapo katika kipindi Cha miaka miwili serikali ya awamu ya sita imeleta watumishi, imejenga zahanati, vituo vya afya pamoja na majengo ya huduma za dharura katika mkoa wa Simiyu

Pia ameendelea kuwaasa wananchi wa Maswa kuwa hawana haja ya kukimbilia sehemu zingine kupata huduma ya dharura kwa kuwa serikali imesogeza huduma hiyo karibu ili kuwahudumia. Pia alisema vituo vyote vilivyojengwa vianze kutoa huduma na serikali ya awamu ya Sita italeta magari mawili kwa ajili ya kutoa huduma za wagonjwa na lingine kwa ajili ya kufanya huduma shirikishi.

Pia  Waziri mkuu amekagua kiwanda Cha chaki kilichopo kitongoji cha Ng'hami katika Kata ya Nyalikungu ambacho ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 8 mpaka sasa na mkandarasi aliyetekeleza mradi huo ni Suma JKT na ameutaka uongozi wa halmashauri kusimamia kiwanda hicho ili kianze kuzalisha chaki na kutoa ajira na kuongza mapato ya serikali.

Mhe. Waziri Mkuu  akipata maelezo namana kiwanda kinatakavyo fanya kazi za uzalishaji wa chaki

Mtambo wa kuchakata chaki katika Kiwanda cha Chaki Ng'hami Maswa

Mtambo wa kuchakata chaki katika Kiwanda cha Chaki Ng'hami Maswa

Sambamba na hayo pia amekagua ujenzi wa reli ya kisasa awamu ya tano kipande cha kutoka Isaka mpaka Mwanza chenye urefu wa KM 341 ambapo gharama ya ujenzi huo ni Dora bilioni 1.326 sawa na shilingi tilioni 3.062 mpaka sasa ujenzi huo umefikia asilimia 28.05 na wafanyakazi zaidi ya 6721 ni watanzania wakati  Simiyu peke yake ikiwa na vijana zaidi ya  520 waliopata ajira katika mradi huo.

Mhe. Waziri Mkuu akikagua ujenzi wa Reli ya mwendo kasi kipande cha Isaka Mwanza katika eneo la Malampaka 26.03.2023

Akizungumza katika nyakati tofauti waziri Mkuu amesema serikali ya awamu ya sita inaendelea kutekeleza maelekezo ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika kuwaletea wananchi maendeleo, kusikiliza kero na kuzitatua.

“Nataka niwahakikishie tutafanya kazi ya kumsaidia Rais wetu usiku na mchana, wakati wa jua na mvua kali, hiyo ndio dhamira yetu ili tuweze kuwafikisha mahali pazuri"

Mhe Kassim Majaliwa amesema watumishi wa Halmashauri wanatakiwa kuongeza Kasi katika utoaji wa huduma kwa kuwafikia wananchi, kusikiliza kero zao pamoja na kutatua changamoto za wananchi

Aidha waziri Mkuu ametoa wito kwa watumishi wa Halmashauri kutoa elimu kwa wananchi kuhusu fursa hizo kwa kuwa kituo kikubwa Cha reli kitavutia wananchi wengi kujenga pia amesema fursa zinakuja katika mradi huo, hivyo amewataka wananchi kuwekeza katika hoteli na gesti.

Kujenga eneo kubwa la kuweka maroli ili kuongeza ajira katika eneo hilo kwa sababu kituo hicho ni kikubwa ambacho kitahusisha kubeba na kushusha mizigo kwa kuwa reli hiyo ni ya kimataifa hivyo tatizo la usafiri litakuwa historia pia amewataka Halmashauri kupima maeneo yanayozunguka eneo hilo ili waweze kupatiwa maeneo yaliyopimwa ili wawe na hati miliki.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.