• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Waziri aridhishwa na ujenzi wa barabara ya mchepuko (by pass) Maswa

Posted on: October 7th, 2023


Waziri wa Ujenzi Mhe Innocent Bashungwa amewapongeza wakazi wa Maswa kwa kupata mradi wa barabara ya mchepuko (By pass) yenye urefu wa kilometa 11.3 ambapo serikali ya awamu ya sita ilitoa Fedha kiasi cha shilingi bilioni 13.4  kwa ajili ya ujenzi huo lengo likiwa ni kupunguza msongamano  wa magari  kwa wananchi wa Maswa hususani mjini.

Amezungumza hayo leo tarehe 07.10.2023 wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua barabara ya mchepuko maarufu by pass ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami katika wilaya ya Maswa Mkoani  Simiyu.

Pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu kwa kuwajali watanzania ambapo  ametoa  kibali  cha shilingi bilioni 16.2 kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi  ambao mtandao wa barabara ulipika katika maeneo yao.

Aidha Mhe Bashungwa amempogeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi ambayo anaifanya ya kujenga mitandao ya barabara nchi nzima, madaraja ya kimkakati pamoja na miradi mingine inayotekelezwa na wizara hiyo

Pia  Waziri wa Ujenzi amepokea ombi la wabunge wa majimbo yote mawili ya Wilaya ya Maswa kuhusu ujenzi wa barabara itakayounganisha Maswa mpaka Malampaka ambapo kituo kikubwa cha reli ya kisasa kinajengwa Malampaka lengo likiwa ni kuwawezesha wananchi wa maeneo mbalimbali kufika kwa urahisi.

"Kutokana na umuhimu wa barabara hiyo kipande hiki cha takribani kilometa 10 kinachounganisha mji wa Maswa na reli ya kisasa mpaka Malampaka, sasa sisi wawakilishi wa Rais tuchukue ombi lenu na kulipeleka kwa Rais na kuelezea umuhimu na mkakati mzuri wa kuunganisha mji wa Maswa na kituo kikubwa cha reli ya kisasa  ili huduma  ya SGR itakapokuwa inapita eneo hilo basi mizigo itakayokuwa inapakuliwa  pale na abiria waweze kufika Maswa na kuendelea na safari sehemu nyingine". amesema Mhe Bashungwa

Mhe Bashungwa amewasisitiza wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya kusimamia miundombinu ya barabara kwa kuhakikisha wote wanaohujumu miundombinu ya barabara hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao na wizara itashirikiana nao kuhakikisha wahalifu wote wanakamatwa.

Pia ametoa wito kwa wakandarasi wote  wakiwepo wazawa kuwa serikali itahakikisha inafanya kazi na wakandarasi wote ambao watafanya kazi kwa weredi kwa mujibu wa mkataba ambao wamekubaliana na serikali kupitia wizara ya ujenzi.

Nae Meneja wa Tanroad Mkoa wa Simiyu Mhandisi John Mkumbo amesema barabara hiyo iko katika hatua za mwisho ambapo mpaka sasa imekamilika kwa asilimia 99  na  vitu vichache vimebaki ili ikamilike ikiwepo uwekaji wa alama barabarani pamoja na vibao vya pembeni.



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.