• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANAWAKE NA VIJANA WAJASIRIAMALI MASWA WAPATA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA, UUNDWAJI NA USAJILI WA VIKUNDI

Posted on: April 16th, 2024

Wanawake na vijana wajasiriamali wilayani Maswa Mkoani Simiyu wamepata mafunzo ya elimu ya fedha pamoja na uundwaji na usajili wa vikundi ili kuwawezesha kupata mikopo isiyo na riba.

Hayo yamezungumzwa na Afisa mahusiano benki ya CRDB tawi la Maswa Ndugu Matensa Lugumba wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Maswa yaliyohusisha wanawake na vijana wajasiriamali wa wilaya ya maswa.

Ndugu Lugumba amesema kuwa lengo la benki hiyo ni kuinua uchumi wa wananchi waliopo Maswa na Taifa kwa ujumla kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine ili kuondokana na mikopo ya kausha damu kwa kuwa mkombozi amepatikana ambaye ni CRDB benki.

Ameongeza kuwa benki ya CRDB kupitia huduma ya CRDB foundation wamekuja na huduma ya iMBEJU ambapo huduma hiyo ni kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake kupitia kwenye vikundi ambapo mikopo hiyo itaanzia shilingi 200,000 mpaka shilingi milioni 5,000,000 na itatolewa bila riba.

Lengo la mikopo hiyo ni kuwainua vijana na wanawake kibiashara ambapo ili mjasiriamali apate mkopo huo ni lazima awe amesajiliwa katika kikundi ambapo benki itaingia mkataba na kikundi kwa ajili ya kumdhamini mjasiliamali atakayehitaji mkopo.

Pia amesema kikundi lazima kiwe na akaunti ya CRDB ambapo kikundi hicho kinatakiwa kiwe na wanachama hai ambao ni waadilifu, wanaofahamiana na wenye malengo thabiti ambayo yataweza kuzaa na kuleta faida.

Ameongeza kuwa mwanakikundi anaweza kupata mkopo moja kwa moja CRDB  ilimradi wadhamini wake ni kikundi ampabo viongozi wao watakuwa wamemsainia na awe anajishughulisha na shughuli yoyote ya ujasiriamali.

Kwa upande wake Afisa vijana kutoka Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Ndugu Berther Lugenji amesema sifa za mjasiriamali anatakiwa kuwa mbunifu mwenye nidhamu ya fedha, mwenye kusimamia mawazo aliyonayo, kujua namna ya kutafuta masoko na kutumia changamoto kuwa fursa katika ujasiriamali anaoufanya ili kufikia malengo.

Nae Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Rodgers Lyimo amewataka wafabiashara ndogondogo kufika katika Ofisi ya Maendeleo ya jamii kwa ajili ya kujisajiri ili waweze kupata vitamburisho vya ujasiriamali ambavyo vitadumu kwa miaka mitatu.

Pia amewashukuru benki ya CRDB kwa kutoa elimu hiyo ambayo itawasaidia vijana na wanawake wajasiriamali kupata mikopo katika benki hiyo sambamba na hilo amewasisitiza wajasiriamali hao kuchangamkia fursa hiyo kwa kuunda vikundi na kufungua akaunti ili wapate mikopo hiyo isiyokuwa na riba.

Lucy Misinzo ambaye ni afisa maendeleo ya jamii amesema kuna aina mbili ya usajili wa vikundi ambapo kuna usajili wa vikundi vya kijamii na kifedha ambapo ili vikundi vya kijamii visajiliwe kikundi  kinatakiwa kiwe na muhtasari wa kuonyesha kikundi kimeadhimia kusajiliwa, katiba pamoja na barua ya maombi iliyopitishwa na Mtendaji wa Kata.

Aidha  ameongeza kuwa ili kikundi cha kifedha kisajiliwe kinahitaji muhtasari, katiba, barua ya maombi na fomu ya azimio la kusajili kikundi cha kifedha pamoja na  mtu atakayekuwa anatoa elimu kuhusu masuala ya fedha.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.