• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Walimu watakiwa kushirikiana ili kuongeza tija katika kufaulisha wanafunzi

Posted on: February 8th, 2023

Maafisa kutoka Divisheni ya Elimu Sekondari Wilaya ya Maswa Mkoa wa Simiyu wamefanya ziara katika shule za Nguliguli Sekondari na Senani Sekondari kuzungumza na Walimu masuala ya taaluma, nidhamu, kutatua changamoto katika mazingira ya kazi na kutambua wanafunzi na walimu wenye mahitaji maalumu.

Akizungumza na walimu hao katika shule hizo Afisa Elimu Taaluma kutoka Divisheni ya Elimu Sekondari Wilaya ya Maswa Ndg. Khalfan Millongo amewaomba walimu kusimamia nidhamu katika shule na kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuongeza ufaulu katika shule zao ziweze kushika nafasi za juu kwenye matokeo ya mitihani ya kidato cha Pili na Cha Nne.

Afisa Elimu Taaluma wilaya  amewapongeza walimu wa Biolojia katika shule ya Sekondari Nguliguli kwa kufaulisha wanafunzi kwa wastani wa C ambayo ni GPA ya 3.35 na walimu wa Kiswahili na Kemia katika shule ya sekondari Senani waliyofaulisha masomo hayo kwa wastani wa GPA ya 3. Kiswahili na Kemia 3.3

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Elimu Maalumu kutoka Divisheni ya Elimu Sekondari wilaya Mwl. Kassongo amewaomba walimu kutoa takwimu za wanafunzi na walimu wenye mahitaji maalumu katika shule hizo ili serikali iweze kuwatambua na kuwawezesha vifaa vya kuwasaidia katika kusikia kutembea na kuona.

Aidha Kassongo amewasisitiza walimu kuwa serikali imeweka mambo muhimu na msingi yasimamiwe ambapo Maafisa wa Elimu Wilaya, Maafisa Elimu Mkoa , Maafisa Elimu Kanda pamoja na Walimu Wakuu wameagizwa kuwa taasisi zote wapande miti ambapo kwa wastani mwanafunzi anatakiwa kuwa na miti kuanzia 3 anayoitunza na wanatakiwa kusimamia kikamilifu.

Serikali imesisitiza kila Shule wahakikishe wanasimamia huduma ya utoaji wa chakula ambapo Kamati za Shule na Bodi wapewe elimu ili washirikiane  na walimu kwa kuwa wabunifu kwa kulima mashamba ambayo yatawasaidia kuzalisha chakula ili kutekeleza majukumu ya serikali na wanafunzi waweze kusoma vizuri ili kuongeza ufaulu kwa sababu wanafunzi watapata chakula eneo la shule.

Kwa upande wao walimu wameomba serikali kuwajengea nyumba maeneo ya Shule ili kurahisisha ufundishaji kwa sababu wanapoishi sasa ni mbali na Shule hivyo kupunguza ufanisi katika kazi yao ya kufundisha na kusababisha ufaulu wa wanafunzi kutokuwa mzuri.

Vilevile upungufu wa walimu wa kike katika baadhi ya shule imekuwa changamoto kwani wanafunzi wa kike wanashindwa kueleza shida zao ambazo walimu wa kike walitakiwa kuzisikiliza pamoja na kuzitatuana ambapo shule 6 za sekondari Wilaya ya Maswa hazina walimu wa kike ikiwepo Nguliguli Sekondari.

Wakijibu changamoto hizo Maafisa Elimu hao wameahidi kuzifanyia kazi changamoto hizo zilizotolewa na walimu na kuwaomba walimu kufanya kazi kwa ushirikiano kuanzia darasani mpaka nje ya darasa ili kuongeza ufaulu na kufuata Sheria na miongozo yote iliyotolewa na serikali katika kutimiza majukumu yao na kusisitiza muda wa michezo uzingatiwe katika shule hizo .


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.