• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata Maswa wapigwa msasa kuhusu jumuiya za kujifuza

Posted on: December 9th, 2023

Wizara ya Elimu, Sayansi na teknolojia kupitia wakala wa maendeleo ya uongozi wa Elimu ADEM imetoa mafuzo ya jumuiya  za kujifunza   kwa walimu wakuu 135 kutoka shule 135 za Wilaya ya Maswa  na Maafisa Elimu Kata 36  yenye lengo la  kujua mbinu mbalimbali za kutatua changamoto na kuongeza ufanisi katika majukumu yao.

Mafunzo hayo yalifanyika kwa siku 4  katika shule ya msingi Shanwa iliyopo Kata ya sola kupitia mradi wa Shule Bora ulifadhiliwa na serikali ya uingereza kupitia mfuko wa UKaid.

Ester Marwa Mratibu wa mradi wa Shule Bora Mkoa wa Simiyu  alitoa wito kwa Maafisa Elimu Kata na Walimu wakuu  kuhusu mafunzo waliyoyapata yakawe chachu ya kuboresha mbinu za uongozi na kiutawala katika ngazi zao za shule na Kata kwa kushirikiana, kuboresha mawasiliano na kutumia lugha nzuri za kiuongozi katika kutoa taarifa ili zilete motisha kwa walimu.

Pia aliongeza kuwa mafunzo yamelenga kuanzisha jumuiya kulingana na jeografia za maeneo Yao ambazo zitawasaidia kukutana mara kwa mara ili kubadilishana uzoefu na kupeana mbinu mpya zitakazowawezesha kushirikiana na kutatua changamoto mbalimbali ili kuleta ufaulu kwa wanafunzi.

"Tunaamini kupitia mafunzo haya yatakuwa ni mwendelezo kwa sababu watakuwa wakikutana katika jumuiya hizi kubadilishana uzoefu na hadithi za mafanikio na Kila mmoja ataiga mazuri hivyo tutaboresha uongozi na walimu watafanya kazi kwa juhudi na kwa moyo na matokeo ya wanafunzi yatakwenda kuboreka sana kutokana na uongozi wa walimu hao". Alisema Mratibu wa Mkoa

Nae  Richard Sungura Mkufunzi kutoka ADEM Mwanza alisema mafunzo hayo yanaenda kuleta mabadiliko makubwa  Wilaya ya Maswa kwa kuwa viongozi wamebeba dhamana ya suluhisho la matatizo yote yanayowakabili walimu na wanafunzi.

" Kiongozi atapimwa kutokana na uwezo wake wa kukabiliana na changamoto, ili uweze kuwa na ufanisi katika kukabiliana na changamoto jitathmini uone wapi umepungua na ujiimalishe na kiongozi hatakiwi kukata tamaa." Alisema mkufunzi Sungura

Afisa Elimu taaluma Wilaya ya Maswa Mwl  Neema Makundi ambaye pia ni Mratibu wa mradi wa Shule Bora Wilaya aliwashukuru programu ya shule Bora na wawezeshaji mahiri kutoka ADEM kwa kuwawezesha walimu mambo mengi ambayo yatakwenda kuleta matokeo chanya katika usimamizi wa Elimu katika maeneo Yao.

Mwl Makundi alisema jumuiya za ufundishaji zitawasaidia kuwaweka pamoja kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika maeneo Yao ya kazi katika usimamizi wa Elimu na kutatua migogoro.

" Mafunzo haya yamekuja katika wakati muafaka kwa maana katika shule zetu changamoto ni nyingi ukisimama peke yako huwezi kufanya, lakini  mnapokaa na mkashirikiana pamoja mna uwezo wa kufanya vizuri zaidi." Alisema mratibu wa mradi Wilaya

Kwa upande wake Mwl Emmanuel Makoye kutoka shule ya msingi Kakola aliishukuru progamu ya shule Bora kwa kuleta mafunzo hayo ya jumuiya za ujifuzaji kwa kuwa inaenda kuwa tiba ya kutatua migogoro kwa sababu jumuiya hizo  zitaleta umoja na mshikamano baina yao

Mwl Ada  Dizaya kutoka shule ya msingi Mkapa iliyopo Kata ya Kadoto alisema mafunzo hayo yamemjengea uwezo wa kwenda kufanya vizuri zaidi katika kituo chake Cha kazi na jamii inayonzunguka kwa sababu ataweza kutatua changamoto mbalimbali kwa  sababu amejifunza mbinu mbalimbali kwa ufanisi.

"Mimi nafurahi sana kupata mafunzo haya, na mafunzo haya yaendelee ili kusudi yaweze kutusaidia na kutupa Elimu zaidi lengo kuu kuinua Elimu kama lengo lilivyokusudiwa." alisema mwl Dizaya


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.