• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Walimu wa shule za msingi Simiyu wanufaika na mafunzo ya mbinu mpya za stadi za KKK

Posted on: February 18th, 2023

Walimu wa shule za msingi Mkoa wa Simiyu wamepata mafunzo ya mbinu bora za ufundishaji  yanayotolewa na mradi wa Elimu bora kuwasaidia walimu hao kumudu stadi za ufundishaji wa watoto wa darasa la Awali, darasa la Kwanza na darasa la Pili katika Kusoma, Kuhesabu na Kuandika (KKK).

Mafunzo hayo yanafanyika siku tano katika shule ya msingi Shanwa katika Halmashauri ya ya Wilaya ya Maswa ambapo walimu 120 kutoka shule 40 zinazofanyanyiwa majaribio na mradi huo wa Elimu bora zimeleta walimu watatu ambao wanafundisha madarasa ya awali, darasa la kwanza, na darasa la pili katika shule hizo kupata mafunzo.

Nae Afisa Taaluma Mkoa wa Simiyu William Mapunda  amesema  walimu hao wanaopata mafunzo hayo watatumika kufundisha walimu waliopo katika shule zingine kwenye Wilaya zao kwa kuwa wamepata mbinu nyingi mpya za namna ya kufundisha darasa lenye watoto wengi na tatizo la watoto kutokujua kusoma litakuwa limeisha kabisa.

"Malengo hapa hasa ya serikali ni kuhakikisha watoto hawa wanamudu stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu wakiwa bado kwenye madarasa ya chini kabla hawajafika madarasa ya juu hasa darasa la nne ambapo wataenda kufanyiwa upimaji wa namna walivyoweza kumudu hizo stadi" amesema Mapunda.

Kwa upande wake Afisa Mitahara kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania ambaye ni mratibu wa mafunzo ya  mradi wa shule bora Ndg. Emmanuel Stanslaus amesema mafunzo  hayo yamefanyika ikiwa bado kuna changamoto katika stadi hizo tatu za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) hivyo mradi unaendelea kutoa mafunzo hayo lengo likiwa ni kuwasaidia walimu wa madarasa hayo kuweza kumudu stadi za ufundishaji kwa watoto wa darasa la awali, darasa la kwanza na darasa la pili.

Katika hatua nyingine walimu wameishukuru serikali kupitia mradi wa shule bora kwa kuwaletea mafunzo hayo ambayo yamewasaidia kujua mbinu mbalimbali mpya ambazo watazitumia katika ufundishaji wao ili kuimarisha maarifa ambayo yatamsaidia mwanafunzi huyo wa darasa la awali, darasa la kwanza na darasa la pili kuelewa kwa haraka.

Pia walimu wamesema mafunzo hayo yamekuja wakati sahihi na kupitia mafunzo hayo walimu hao wamebaini mbinu ya kuwatambua watoto wenye mahitaji maalumu ambao watakuwepo katika madarasa wanayofundisha wito wao kwa serikali ni kuiomba iendelee kuleta mafunzo hayo ili yawajenge zaidi katika stadi hizo.

Mafunzo hayo pia yamelenga kuwashirikisha wazazi ambapo walimu wamefundishwa mada  ambazo zitamuwezesha mzazi kushiriki katika kuboresha ufundishaji na wao kuwa sehemu ya kusaidia serikali kupata matokeo bora.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.