• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Walimu mkoani Simiyu wapata Mafunzo ya Elimu jumuishi

Posted on: August 7th, 2023

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  kupitia Taasisi ya Elimu Nchini imewawezesha Walimu wapatao (50) kutoka shule za msingi 50 kupata mafunzo ya ufundishaji na ujifunzaji jumuishi.

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa muda wa siku 4 ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kupitia program ya Shule Bora yamefadhiliwa na Serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UKAID.

Ester Marwa Mratibu wa Elimu bora ngazi ya Mkoa alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuinua kiwango cha elimu jumuishi pamoja na kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia.

Marwa aliongeza kusema kuwa mafunzo hayo yanawajengea uwezo Walimu kuweza kuwatambua watoto wenye mahitaji maalumu na kujua mbinu rafiki na jumuishi za kujifunzia.

“Mkoa kwa sasa una zaidi ya wanafunzi (605) wenye mahitaji maalumu na mwaka huu 2023 pekee tumeandikisha wanafunzi 234, hivyo unaweza ukaona ambavyo elimu bora ilivyochangia kuongeza usajili wa wanafunzi”Alisema Marwa.

Mwl Neema Makundi Afisa Elimu taaluma Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na Mratibu wa Elimu bora Wilayani Maswa alisema kuwa anaishukuru Serikali kwa kuwaletea mafunzo hayo kwa kuwa yatasaidia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kuweza kujifunza.

“Mafunzo haya yanawasaidia walimu kujua mbinu za kujifunza maana wamefundishwa mbinu za kufundishia na namna ya kutengeneza  zana za asili za kujifunzia ili watoto wote waweze kupata fursa ya kujifunza”.Alisema Makundi.

Mwl Salimu Kidunda kutoka Shule ya Msingi Nyasosi Kata ya Ngulyati Wilayani Bariadi Mkoani hapa alisema kuwa mafunzo hayo yamesaidia kuandaa dhana za kufundishia na kuwatambua watu wenye mahitaji maalumu.

“Mafunzo haya yamenisaidia kujua makundi ya watu wenye ulemavu na kujua alama za kufundishia kwenye elimu jumuishi na kuweza kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalumu kuweza kuzifikia ndoto zao.”Alisema Kidunda.

Mwalimu Ferister Mkenda toka Shule ya Msingi Budalabujiga “A” alisema kuwa mafunzo haya yametusaidia walimu kwenda kuwasaidia wazazi walio na watoto wenye mahitaji maalumu.

“Kama walimu tumefundishwa kwenda  kuwa daraja kati ya wazazi na kuwapa elimu juu ya umuhimu wa elimu ili wazazi waone umuhimu wa kusomesha watoto wenye mahitaji maalumu”.Alisema Mkenda.

Nae  Kisandu Mkazi wa Biafra Wilayani hapa alisema kuwa anaishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya watoto wenye mahitaji maalumu kuweza kujifunza, huku akitoa rai kwa Serikali kuweza kuongeza walimu.

“Tunaishukuru Serikali kwa kuboresha miundombinu ila tunaiomba Serikali iongeze walimu, kwa mfano Shule ya msingi Binza inamwalimu mmoja anaefundisha watoto wenye mahitaji maalumu kuna wakati watoto wetu hawapati masomo inapotokea Mwalimu anaudhuru.”  Alisema Mzazi huyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.