• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wakulima wa Pamba kupata mbegu na viuatilifu bure

Posted on: July 10th, 2023

Balozi wa Pamba Tanzania Mhe. Agrrey  Mwanri amesema  Serikali imepanga kuleta mbegu na viuatilifu bure kwa wakulima wa pamba lengo likiwa ni kupunguza makali ya  soko ambalo limewaathiri kwa mwaka huu pamoja na kutoa elimu ya namna bora ya kulima kwa kufuata kanuni za kilimo cha pamba ikiwepo kuandaa shamba mapema baada ya msimu wa mavuno kukamilika.

Balozi wa pamba nchini Tanzania Mhe. Agrrey Mwanri amewataka wakulima wa pamba kuzalisha kwa wingi zao hilo kwa ubora unaotakiwa ili liwe na tija katika soko la Dunia ambapo katika msimu huu zao hilo limelimwa kwa wingi na  nchi nyingi Duniani hivyo kusababisha mdololo wa bei katika soko.

Aidha balozi wa pamba alisema msimu uliopita bei ya pamba ilikuwa juu kutokana na wazalishaji wengine huko Duniani hawakulima pamba kutokana na COVID-19 hivyo kufanya bei iwe juu tofauti na sasa ambapo nchi zote ambazo hazikuzalisha  zao hili kipindi hicho zimezalisha msimu huu na kusababisha pamba kuwa nyingi.

Mhe. Mwanri amesema hayo katika Halmashauri ya Wilaya  ya Maswa  katika ziara yake katika Kijiji Cha Buyubi na Dodoma katika Kata ya Mwamashimba wakati akiwa katika mkutano wa Kijiji kwa lengo la  kuwaelimisha wakulima wa pamba namna bora ya kuvuna pamba nzuri ambazo zitaweza kupata soko kimataifa kutokana na ubora wake.

“Tukizalisha pamba nyingi hapa na bei ikaanguka kule duniani bado hela yetu itakuwa nyingi kwa sababu itakuwa na ubora na wingi unaotakiwa kulinganisha na bei iliyopo”  amesema balozi wa pamba.

Pia amewataka wakulima kushirikiana kila mmoja kusimama kwenye nafasi yake kwa kuelimishana wao kwa wao jinsi ya kulima pamba ili kujipatia fedha nyingi.

Nae Diwani wa Kata ya Mwamashimba  Mhe.  Saida Daudi Dila amewataka wananchi kuzingatia elimu waliyopewa na Balozi wa pamba kwa lengo la kumkomboa mkulima kiuchumi kwa kupata elimu ya kanuni bora za kilimo cha pamba.

Pia Mheshimiwa Diwani amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa pampu za kupulizia wadudu pamoja na viutalifu bure, hivyo amewaomba wananchi kutumia fursa hizo ambazo Rais amewapa ili ziwasaidie katika shughuli zao.

Aidha amewasisitiza wananchi wake kuvuna pamba kwa kufuata  kanuni ili kuepuka pamba chafu ambazo hazistahili katika soko hivyo kusababisha kipato chao kushuka na kukosa wanunuzi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Maisha Mtipa  amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwawezesha wakulima wa pamba kwa hali na mali kwa kutoa pembejeo na mbolea ambazo zitawasaidia kujipatia kipato watakapovuna pamba yao.

Mkuu wa Wilaya ameishukuru Serikali pamoja na Mkurugenzi wa bodi ya Pamba Tanzania kwa kumleta Balozi wa Pamba katika Wilaya ya Maswa kwa kutoa elimu ambayo imekuwa chachu kwa wakulima wa pamba kuanza kutumia kanuni bora za kilimo cha pamba na kuzalisha kwa tija.

Pia Mhe. Kaminyoge amewataka watendaji wote kuanzia ngazi ya Halmashauri kusimamia kwa karibu wakulima wa pamba kwa kutoa Elimu kuhusu kanuni bora na Sheria ili kuzalisha kwa tija zao hilo.

Halmashauri inatarajia kulima Jumla ya Hekta 82,212.4 za zao la pamba katika msimu wa Kilimo wa 2022/2023 na kutarajia kupata mavuno ya Tani 102,765.06, mpaka kufikia mwishoni mwa msimu wa Kilimo Cha pamba jumla ya Hekta 87,438.06 za zao la pamba zimelimwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambapo ni sawa na asilimia 106.35.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.