• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wadau mbalimbali wapata Elimu kuhusu masuala ya maafa

Posted on: October 26th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amewataka wadau  wote wa maafa kutoa Elimu kwa wananchi kuchukua tahadhari kuhusu maafa lengo likiwa ni kuwajengea uelewa wananchi namna ya kujilinda pindi mvua hizo zitakapoanza.

Pia mkuu wa Wilaya amewataka wananchi kuimalisha nyumba zao na kuchukua tahadhari na hatua madhubuti kwa kuhakikisha watoto wao wanakuwa karibu na makazi yao pindi watakapoona dalili za mvua kuanza.

Ameongeza kuwa katika msimu huu mvua za vuli zitanyesha kuanzia mwezi Oktoba hivyo Mamlaka ya hali ya hewa imetoa utabili kuwa mvua zitanyesha juu ya wastani ambapo zitasababisha madhara kwa watu na miundombinu.

Mkuu wa Wilaya amesema hayo katika kikao kazi cha kamati ya maafa kilichowashilikisha wadau mbalimbali kutoka taasisi mbalimbali za kidini, mashirika yasiyo ya kiserikali taasisi za kiserikali, wataalamu pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

"Kama watendaji wa umma tuna kila sababu ya kuchukua maelekezo ya Rais na kuwatahadhalisha wananchi juu ya jambo hilo, na kama maafa yakiwakuta tuna kila sababu ya kuchukua hatua kuhakikisha tunawanusuru uhai na Mali zao, tuna kila sababu ya kunusuru miundombinu mbalimbali itakayoathirika na jambo hilo, miundombinu ya barabara, afya, Elimu, na maji." Amesema Mkuu wa Wilaya

Pia mkuu wa Wilaya amewataka viongozi wawe wepesi wa kutoa taarifa linapotokea tatizo kwa kushiriki pamoja kunusuru sehemu ambazo maafa hayo yametokea kuliko kusubiri viongozi wa juu kwenda kutatua changamoto hiyo.

Aidha Mhe Kaminyoge ametoa wito kwa Mamlaka mbalimbali ikiwepo wakala wa barabara za mijini na vijijini (TARURA), wananchi waliopo mjini, pamoja na Mamlaka zingine zote  kuhakikisha wanasafisha mifereji yote iliyopo mjini mpaka eneo ambalo maji hayo yanaenda katika mito ili kuepusha wananchi kupata mafuriko.

"Endapo maafa yametokea mahali, hatua ya kwanza ni kutoa taarifa kwa ngazi zote kuanzia ngazi ya chini mpaka ngazi ya juu kwa kuchukua hatua kwa kadri ya uwezo walionao kama ni serikali ya Kijiji basi wananchi waungane na viongozi kuweza kuwasaidia wananchi waliopata maafa hayo wakati serikali inajulishwa." Mhe. Kaminyoge amesema

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Vivian Christian ametoa mwezi mmoja kwa  watendaji wa Kata wawaelimishe  viongozi wengine sambamba na wananchi kuhusu namna ya kuchukua tahadhari dhidi ya maafa ili wananchi wawe na uelewa huo.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe. Paul Maige amesema jukumu kubwa la viongozi ni kuhakikisha wananchi wanakuwa salama endapo maafa yatatokea kwa kuwa watendaji wanayajua maeneo yao vizuri ambayo yalikuwa yanatumika kwa Kilimo na sasa ni makazi endapo kutatokea maafa ofisi ya Mkurugenzi ipate taarifa mapema ili iweze kuchukua tahadhari mapema.

Katika kikao hicho kamati ya maafa ilitoa mada mbalimbali kuhusu masuala ya maafa ambazo zitawasaidia washiriki kuwaelimisha wananchi kuchukua tahadhari katika kipindi hiki cha mvua ambazo zitanyesha juu ya wastani.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.