• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VITENDO VYA UKATILI MASWA VYAPUNGUA KUTOKA 671 HADI KUFIKIA 591 MWAKA 2024

Posted on: December 10th, 2024

Vitendo vya ukatili katika Wilaya ya Maswa vimepungua kutoka 671 mwaka 2023 hadi kufikia  591 kwa mujibu wa rekodi za kuanzia mwezi januari hadi mwezi Desemba mwaka huu.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa Ndg Athuman Kalaghe akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Maswa alisema kuwa maadhimisho hayo ni kuikumbusha jamii kupinga ukatili unaoendelea katika jamii zao ambapo serikali imetunga sera, sheria na miongozo mbalimbali itakayosaidia kutokomeza  ukatili wa kijinsia.

Pia Ndg, Kalaghe alitoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanatoa taarifa haraka za ukatili kwa wataalamu waliopo katika maeneo yao ili wale waliofanyiwa vitendo hivyo wapate msaada.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema “Kuelekea Miaka 30 ya Beijing chagua kutokomeza ukatili wa kijinsia”

Aliongeza kuwa kauli mbiu hiyo inasisitiza mtu binafsi na jamii kwa ujumla kuchukua hatua madhubuti za kupinga, kukataa na kukemea ukatili wa kijinsia na kutoa nafasi kwa kila mtu kufanya tathmini kuelekea  miaka 30 ya kupinga ukatili.

Pia Katibu Tawala alieleza  kuwa takwimu  zinaonyesha vitendo vya ukatili vinatokea zaidi kwa wanawake na watoto ikiwa ni kundi linalopitia changamoto nyingi za ukatili kutokana na mgawanyiko usio sawa wa majukumu katika familia hivyo ni muhimu sana kuimarisha maendeleo na ustawi wa watoto ili kupunguza changamoto zinazowakabili.

Katibu Tawala alieongeza kuwa uwepo wa vitendo vya ukatili unapelekea kuwa na ulemavu wa kudumu, mimba za utotoni, magonjwa mbalimbali ya kuambukiza, vifo, matatizo ya kisaikolojia, kujiua, umaskini uliokithiri pamoja na kupoteza nguvu kazi.

Aidha alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kutokomeza ukatili wa kijinsia ikiwemo kampeni maalumu 16 za kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Akitoa taarifa Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Maswa Bi. Lilian Clement alisema kuwa sababu za kupungua kwa vitendo hivyo vya ukatili ni  kutokana na Halmashauri ya Wilaya kwa  kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwepo Shirika la World Vision, Ustawi wa Jamii, Divisheni ya Maendeleo ya Jamii pamoja na Radio SIBUKA  kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa wananchi.

Maadhimisho hayo ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yalifanyika Kiwilaya katika Kata ya Senani ambapo kata nne zilihudhulia maaadhimisho hayo ikiwepo Ngulinguli, Mpindo, pamoja na Mwamanenge tarehe 10 Desemba, 2024.

 Ameeleza kuwa  Katika maadhimisho hayo  kazi zilizofanyika  katika siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilikuwa ni kutoa elimu  Redio SIBUKA, kutoa elimu katika Hospitali ya Wilaya kutoa elimu kupitia mikutano ya hadhara kwa Kata za Shishiyu, Kadoto na Jija, kutoa elimu mashuleni pamoja na maeneo mengine.

Pia aliongeza kuwa takwimu za ukatili zimepungua kutokana na matokeo chanya ya harakati za mapambano hayo kutoka kwenye mamlaka na wadau.

Kwa upande wake meneja mradi wa REACT-IN Dr. Stanford Kaserwa alisema shirika la world vision  kupitia mradi wa REACT-IN kwa kushirikiana na serikali wameendelea kupambana na vizuizi hivyo kwa kuiwezesha jamii kubadili mitazamo katika masuala ya usawa wa kijinsia na masuala ya ukatili kwa ujumla katika sekta ya afya na lishe.

Pia alibainisha kuwa World Vision inashirikisha wanaume na vijana wa kiume wawe chachu katika jamii kupinga ukatili wa kijinsia.





Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.