• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

UHAMASISHAJI WA WANACHI KUZINGATIA MATUMIZI BORA YA VYOO MASWA

Posted on: January 14th, 2025

Timu ya Hamasa na Uhamasishaji ikiongozwa na Msanii Mahiri ambaye pia ni Balozi wa Taasisi ya Mtu ni Afya ambayo ipo chini ya Wizara ya Afya Ndg. Mrisho Mpoto imefanya ziara ya siku mbili Wilayani Maswa yenye lengo la kuhamasisha na kutoa elimu ya mtu ni afya kwa wananchi wa wilaya ya Maswa  hususani elimu ya kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu.

Lengo la kampeni ya mtu ni afya ni kuelimisha wananchi  kuhusu magonjwa na hatari za kiafya kwa malengo ya kuzuia na kuhimiza wananchi kudhibiti afya zao.

Balozi huyo amezungumza na wananchi wa Kata za Sangamwalugesha, Shanwa na Malampaka kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara  ambapo ametoa elimu  ya namna ya kujikinga na ugonjwa wa kipindupingu kwa kuzingatia ujenzi na matumizi bora ya vyoo majumbani, makanisani maeneo ya mikusanyiko pamoja  na misikitini.

Pia unawaji wa mikono kwa maji tiririka na sabuni  kwa kuzingatia hatua tano za unawaji nyakati zote mtu anapotoka chooni.

Balozi, Mpoto  amegawa masinki ya vyoo, ndoo za maji na matisheti kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kutumia vyoo bora ambavyo vitasaidia kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu.

Kwa upande wake Musa Maduhu mkazi wa kijiji cha Sangamwalugesha ameuomba uongozi ngazi ya afya kuwafuatilia kwa ukaribu watu wote ambao hawana vyoo ili wachimbe na kutengeneza vyoo bora ili kuondokana na kipindupindu.

Nae Tadeus Shija Mchungaji wa kanisa la EAGT Sangamwalugesha ameishukuru timu ya hamasa  ikiongozwa na balozi mpoto kwa elimu waliyoitoa na amewashauri wananchi wenzake kuacha kuogelea kwenye mabwawa na mito  kwa kuwa maji hayo  hayana usalama kwa kuwa yanatoka sehemu mbalimbali na kusababisha mtu huyo anayeogelea kupata kipindupindu.

Godfrey masanja mkazi wa Sangamwalugesha ameishukuru serikali kwa kutenga muda kwa ajili ya kutoa elimu na pia akatoa maoni yake ili kipindupindu kiweze kuisha ni lazima kuwe na mpangokazi wa kutembelea nyumba kwa nyumba kutoa elimu kupitia  kamati ya ustawi wa jamii.

Regina Masanja mkazi wa Malampaka amewataka wananchi wa Malampaka kuhamasishana wao kwa wao na pia uongozi wa kijiji kuunda kamati ya afya kuwatembelea wananchi hao 36 ambao hawana vyoo ili waweze kujenga vyoo.

Amina Hamisi mkazi wa Malampaka ametoa wito kwa wananchi wenzake wakawe mabalozi wa kujenga vyoo bora katika kaya zao ili kuweza kutokomeza kipindupindu katika Kata ya Malampaka.

Takwimu zinaonyesha katika Kata ya Sangamwalugesha ina zaidi ya kaya 1,624 ambapo kaya zenye vyoo bora 643, kaya zenye vyoo vya shimo 945 na kaya ambazo hazina vyoo ni 36, katika Kata ya Malampaka ina jumla ya kaya 2,779 kaya zenye vyoo bora ni 1,583 kaya zenye vyoo vya asili ni 1,159 na kaya ambazo hazina vyoo ni 37.





Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.