• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Uhamasishaji wa kilimo bora cha pamba

Posted on: December 23rd, 2022

Kampeni ya uhamasishaji wa elimu bora ya kilimo cha pamba umefanyika katika Wilaya ya Maswa lengo likiwa ni kuwaelimisha wakulima wa pamba kanuni bora za kilimo hicho ili waweze kulima kwa tija na kuongeza uchumi wa mkulima, wilaya na taifa kwa ujumla. Uhamasishaji huo umefanyika kwa siku 5 katika Wilaya ya Maswa.

Halmashauri ya wilaya ya maswa ina majimbo mawili ya uchaguzi ambayo ni Maswa Mashariki na Maswa Magharibi yenye Kata 36, Vijiji 120 na Vitongoji 510 wakulima wa pamba katika Wilaya ya Maswa wapo zaidi ya 92,000 ambao kwa wastani wanalima heka 1 na kuendelea.

Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa Mikoa inayozalisha Pamba kwa wingi hivyo  kwa umuhimu huo serikali  imeagiza Mkoa wa Simiyu kufikia 2025 iwe na uwezo wa kuzalisha Tani zipatazo 500,000 za pamba na Wilaya ya Maswa inatakiwa kuzalisha  Tani 130,000 ifikapo mwaka 2025 kwa kuwa ni Wilaya ya pili kimkoa inayozalisha pamba kwa wingi.

Ili kutilia mkazo katika zao hilo bodi ya pamba Tanzania chini ya balozi wake Mhe. Agrrey Mwanri imemlika katika Wilaya  hiyo ya Maswa kuongeza nguvu kwa kutoa Elimu ya kanuni bora za kilimo cha pamba ambazo zitaongeza tija katika kilimo hicho na kumfanya mkulima kuzalisha kilo 2,000 kwa heka moja endapo atafata kanuni bora za kilimo cha kisasa cha zao la pamba ambalo litamwinua  mkulima katika uchumi wake na kuongeza mapato ya Wilaya, mtu, kaya na familia kwa ujumla.

Kuna hatua  mbalimbali ambazo mkulima anatakiwa kupita katika uzalishaji wa zao hilo la pamba.

Namna ya kuandaa shamba la  pamba

Ng'oa masalia yote ya pamba ya msimu uliopita na ukusanye katikati ya shamba na kuyachoma moto hii itasaidia kuepukana na wadudu wote kama vile chawajani katika msimu mwingine wa kilimo.

Lima shamba lako mapema na tarehe ya  kuanzia kupanda  ni mwezi novemba tarehe 15 mpaka disemba 15 ili kuepusha pamba yako kuingiliwa na wadudu wakati wa ukame wa kuanzia mwezi  Januari.

Lima shamba lako baada ya siku 3 vuruga tena au Lima shamba hilo tena tayari kwa kupanda mbegu kwa kuwa litakuwa limepoa.

Tumia vipimo vya kisasa vya kilimo cha pamba ambavyo ni sentimita 60 mstari kwa mstari  au pima rula mbili ambayo itakuletea sentimita hizohizo 60, na sentimita 30 mche na mche au rula moja hii itasaidia mkulima kupata Miche 44,000.

Chimba shimo kwa kutumia ncha za jembe na sio jembe lote hii itasaidia mbegu yako kuota vizuri.

Weka mbolea ya samadi au DAP katika shimo ulilochimba na sio kuimwaga tu shambani hiyo itasaidia kutunza unyevu unyevu wakati wa ukame.

Fukia kidogo mbolea yako ili isigusane na mbegu yako kwa kuwa ikigusana itasababisha kuungua kwa mbegu uliyopanda.

Panda mbegu yako ya pamba kwa kila shimo mbegu 3-5 itasaidia kupata mbegu bora zaidi pia kusaidia mbegu kutoka kwa urahisi kuliko ile ambayo utaweka mbegu zaidi ya Tano hautapata mbegu nzuri na itakupotezea muda mwingi kupunguzia.

Mkulima epuka kuchanganya pamba na mazao mengine wakati unapanda mbegu za pamba,  hii itasaidia kuepusha wadudu kushambulia  pamba yako mfano kivuli cha mahindi hufubaza pamba na hivyo hutopata mavuno mengi.

Fukia mbegu yako na ni muhimu kuandika tarehe ya siku uliyopanda mbegu ya pamba.

Mbegu itaota baada ya siku 7 mkulima unatakiwa utembelee shamba lako ili kuona sehemu ambapo haijaota ili urudishie mbegu na sio mche.

Baada ya siku 21 punguzia Miche ibaki 2 tu ambayo itakuwa na rangi ya zambarau na kijani kinachovizia hiyo ndio pamba inayostahili kubaki shambani maana imekidhi vigezo vyote.


Hatua ya palizi

Kuna aina mbili za palizi ambazo ni palizi nzuri na palizi mbaya

Palizi nzuri ni Ile ambayo imekidhi vigezo vya kanuni bora za kilimo cha pamba kwa kufuata vipimo vya sentimita 60 kwa mstari na sentimita 30 mche na mche kuweka mbolea, na nafasi ya kupita wakati wa kupalilia.

Faida za palizi nzuri

 Itasaidia kuongeza ubora wa pamba yako

 Itazuia mmomonyoko wa ardhi

 Itasaidia kufubaza magugu na nyasi kupata katika pamba

Palizi mbaya

Hii ni palizi ambayo haijakidhi kanuni za kilimo bora cha pamba mfano kumwaga mbegu, kutokuweka mbolea na kutokuchimba mashimo.

Athari za  palizi mbaya

 Husababisha mmomonyoko wa ardhi

 Haizalishi Miche mingi

Palizi ya kutumia jembe la wanyamakazi hili ni jembe linalopalilia heka kuanzia 5 kwa siku na inashauriwa mkulima aliyefata kanuni za kilimo bora cha pamba ndio ataweza kutumia ili kurahisishia kazi na linapatikana katika bodi ya pamba hivyo kwa mkulima yeyote anayehitaji aandikishe jina lake kwa afisa ugani wa eneo lake.


Jinsi ya kunyunyuzia

Mkulima wa pamba unashauriwa kuwa endapo utaona wadudu katika shamba lako ni muhimu uchukue hatua za kunyunyuzia sumu katika pamba yako ili kuepusha pamba yako kuliwa na kupunguza uzalishaji.

Namna ya  kunyunyuzia pamba

Pampu zilizotumika katika kampeni ya kutoa Elimu/ kuhamasisha wakulima kanuni bora za kilimo cha kisasa katika kipengele cha unyunyuziaji kulikuwa na aina mbili za pampu ambazo zilitumika ni pampu aina ya MATABI na pampu aina ya ULVA PLUS hizi ndizo pampu zilizotumika kutolea elimu kwa vitendo.

Jinsi ya kuchanganya sumu

Sumu inachanganywa kutokana na ujazo wa sumu ukoje katika chupa maana kila sumu ina ujazo tofautitofauti hivyo mkulima unashauriwa kuangalia katika chupa/ vifungashio hivyo vina milimita ngapi ndio uchanganye sumu yako kwa kufuata utaratibu.

Mfano katika elimu hiyo balozi wa pamba  alitumia sumu aina ya charisma yenye mills 100 ambayo mkulima unatakiwa kugawa mara 3 hivyo utaweka mills 33 kwenye hizo Lita 2 za maji uliyoweka kwenye pampu.

Kisha tikisa mpaka dawa ichanganyike baada ya hapo weka Lita 14 za maji zilizobaki ili kukamilisha Lita 16 tikisa tayari kwa kunyunyuzia.

Mkulima unashauriwa kunyunyizia juu ya mmea na chini ya mmea ili kuua wadudu wote.

Pampu aina ya kadogoo/ Ulva plus hii ni aina ya pampu inayotumia betri nane ambayo inatumika kunyunyuzia pamba kwa njia ya mvuke tu.

Jinsi ya kutumia

Weka Lita 5 za maji

Weka sumu yote katika maji Kisha changanya

Nyunyuzia sumu juu tu kwa kuhesabu mistari 3 kisha mstari wa katikati ndio utapiga sumu yako ambayo itasambaa kwenye mistari mingine 2.

Angalizo

Mkulima unashauriwa kupiga sumu kuanzia saa mbili au saa tatu asubuhi kwa kuwa alfajili bado kuna umande mwingi hivyo wadudu hawatakufa kwenye pamba yako na pia ikifika saa 6 mchana ailisha zoezi hilo mpaka saa 11 jioni ambapo wadudu watakuwa wanaonekana hivyo ni vizuri mkulima wa pamba kuzingatia hilo.

Mkulima anashauriwa kutumia nozeli ambayo ni maalumu kwa pamba na sio kila nozeli ni nzuri kwa matumizi ya kupulizia kwenye pamba.


Jinsi ya kuvuna pamba

Wakati wa kuvuna pamba mkulima wa pamba anatakiwa kuvuna vizuri pamba yake na kuihifadhi kwenye mifuko maalumu ambayo itatolewa na bodi ya pamba bure kabisa ili pamba hiyo ipate soko zuri kimataifa.

Balozi wa pamba amefika Wilaya ya Maswa na kutoa elimu kwa vitendo ya kanuni bora za kilimo cha pamba. Takribani wakulima zaidi ya 5,155 kutoka katika Kata 11 kati ya 36 Vijiji 30 kati ya 120 walitembelewa.  

Wakulima wa Maswa wamefurahia elimu hiyo kwa kuwa itawaletea manufaa na wamemshukuru sana balozi kwa kujitoa kwake kufika Maswa na kuwaelimisha kwa vitendo kanuni bora za kilimo cha pamba na wameahidi watazingatia yote waliyoelekezwa ili wapate pamba nyingi.

Mtaalam  akionyesha namna ya kuchimba mashimo kwa kutumia ncha ya jembe

Mtaalam wa Kilimo pamoja na mkulima maarufu wakionyesha jinsi ya kushika mbegu wakati wa kupanda

Mkulima akionyesha namna ya kupalilia kwa kutumia jembe la wanyamakazi katika shamba

Balozi wa pamba akitoa elimu ya unyunyuziaji kwa kutumia pampu aina ya MATABI

Balozi wa pamba akitoa elimu ya kunyunyuzia kwa kutumia pampu aina ya ULVA PLUS katika  zao la pamba

Balozi akitoa elimu ya jinsi ya kutumia mifuko ya kuvunia na  kuhifadhia pamba wakati wa kuvuna pamba

Mkulima wa pamba akimshukuru balozi wa pamba kwa elimu nzuri waliyoipata ya kanuni bora za kilimo cha pamba



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO March 02, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rc ataka ushirikiano kwa wanawake Simiyu uendelee

    March 09, 2023
  • Walimu Wakuu, Maafisa Elimu Kata na Wenyeviti wa Kamati wapata mafunzo

    March 06, 2023
  • MUAC kutambua watoto wenye matatizo ya lishe

    March 04, 2023
  • DC asisitiza wakulima wote wapatiwe mabomba

    March 03, 2023
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS
  • Mfumo wa MVC-MIS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.