• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Timu ya usimamizi wa pamba yazinduliwa Maswa

Posted on: May 30th, 2023

Katibu Tawala Wilaya ya Maswa ndg Agness A. Alex amezindua rasmi timu ya usimamizi wa ununuzi wa zao la pamba msimu wa 2023 ngazi ya Wilaya yenye jukumu la kusimamia ununuzi wa pamba usafirishaji, kukusanya takwimu za pamba, kutatua changamoto zinazojitokeza wakati wa ununuzi pamoja na kuhakikisha taratibu, sheria na kanuni za ununuzi wa zao la pamba zinafatwa kwenye soko.

Katibu tawala ameyasema hayo wakati akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge  katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya leo tarehe 30.05.2023 na kuhudhuriwa na kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, timu ya usimamizi wa pamba (task force), Afisa utumishi na  watendaji wa Kata.

 Ndg Alex ameitaka timu hiyo ya usimamizi wa pamba ifanye kazi kwa weredi, utiifu na uaminifu ili kusimamia mapato kwa kuwaongezea nguvu watendaji ili kuthibiti mianya ya upotevu wa mapato na pia ameiomba timu hiyo kuepuka kuchukua rushwa wakati wakitimiza majukumu yao kwa kuwa wameaminiwa na wilaya kufanya kazi hiyo.

Aidha Katibu tawala amewataka watendaji wa kata kusimamia na kupita kila wakati kukagua katika mageti hayo ili kuona namna ambavyo kazi inafanyika ya usafirishaji wa pamba

Awali akisoma taarifa hiyo Mkuu wa Idara ya Kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Robert Urassa amesema mageti 15 yameanzishwa ambayo magari yatakuwa yanapita na yakiwa na kibali cha kusafirisha pamba.

Pia amewataka watendaji wa kata kuwahimiza watendaji wa vijiji kuwepo katika maeneo ya ofisi za wanunuzi wa pamba ikiwepo vituo binafsi na AMCOS ambapo  zitasaidia kupata taarifa za Kila siku ya zoezi la ununuzi linaloendelea Katika wilaya ya Maswa ili wawasilishe kwa watendaji wa Kata.

Kwa upande mwingine Katibu Tawala amewataka watumishi kuzingatia kanuni, taratibu, Sheria na muongozo wa mavazi ya utumishi wa umma kwa kuenenda kama mtumishi sambamba na kutunza vifaa walivyopewa kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya kikazi na sio kutumia kwa mambo Yao binafsi kama vile bodaboda.

Pia Ndg Alex amewashauri watumishi  kuwa na nidhamu pamoja na kushirikiana kwa kubadilishana mawazo hiyo itawasaidia watumishi hao kuwa na ufanisi katika kazi kwa kuwa wataweza kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili.

Vilevile Katibu Tawala wa wilaya amewataka watendaji wa Kata kuhamasisha wananchii katika kata zao kufika katika miradi ambapo Mwenge wa uhuru utakapopita uwakute  ili waone  Mwenge  wa Uhuru unavyokagua miradi ambayo Serikali inatekeleza katika Wilaya ya Maswa.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.