• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Tathmini ya Taaluma Wilayani Maswa

Posted on: April 10th, 2019

Leo tarehe 10/4/2019 kimefanyika kikao cha tathmini ya taaluma Wilayani Maswa. Kikao hiki kimehusisha Walimu wakuu, Wakuu wa shule, Walimu mahiri Wilayani hapa, Maafisa elimu Kata, Viongozi wa Elimu ngazi ya wilaya na Mkoa. Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Dr. Seif Shekarage.

Mgeni rasmi amewashauri walimu kulenga mbali kama wanataka kufanikiwa, hii ni kulenga kufaulisha wanafunzi wote na kushika nafasi nzuri kitaifa. Katika suala zima la tathmini imeshauriwa tathmini ianze kufanyika tangu kwa Mwalimu wa Somo.

Pia ameshauri Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule wazieleze Kamati na Bodi za Shule kusimamia suala la upatikanaji wa chakula cha wanafunzi shuleni kwa kupitia uhamasishaji wa  wazazi kuchangia. Wasimamie changamoto ya utoro katika shule zao ikiwa ni pamoja kuorodhesha majina ya Watoto watoro na kuyapeleka kwa afisa Mtendaji wa Kijiji/Kata na siyo Mwalimu kufuatilia hao watoro mwenyewe.

Amewaasa Walimu wasijihusishe na Wanafunzi katika suala la mapenzi kwani ni hatari katika maisha ya kazi yao. Pia ametoa ushauri kwa Walimu kuepuka mikopo isiyokuwa ya lazima kwani inawasababishia matatizo katika familia zao na kuwakosesha amani ya ufanisi wa kazi zao. Kwa msisitizo amesema "Kopeni kwa mpango na katika taasisi za kifedha zinazotambulika"

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa amewaasa Wakuu wa Shule na Walimu wakuu kusimamia suala la nidhamu kwa ujumla katika shule zao kwa kufanya vikao na kuwaelimisha walimu ili kuondoa ombwe la walimu kuingia kwenye matatizo yasiyo ya lazima yanayowasababishia wengine hata kufukuzwa kazi.

Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu ametoa mwongozo wa jinsi gani ya kuboresha elimu kuanzia ngazi ya shule hadi Wilaya. Zinatakiwa kuwepo kamati za taaluma kuanzia ngazi ya shule hadi Wilaya. Kamati hizi zitajumuisha Walimu mahiri wa masomo.

Katibu wa Chama cha walimu Mkoa wa Simiyu amewakumbusha Walimu haki na wajibu wa majukumu yao katika maeneo ya kazi. Aidha ametoa zawadi kwa shule zilizoongoza kwenye matokeo na zilizo kuwa za mwisho. Ametoa zawadi kwa Shule ya Msingi Mwanundi kg.5 za Sukari, Shule ya msingi Nyanguganwa kg.25 za sukari, Shule ya Sekondari Budekwa kg.10 za sukari na Shule ya Sekondari Senani kg.25 za sukari.

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.