• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

TASAF yatoa mamilioni katika Kijiji Cha Mwabujiku

Posted on: April 20th, 2022

Serikali kupitia mfuko wa TASAF imetoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali Wilayani Maswa ambapo Kijiji cha Mwabujiku  kilichoko Kata ya Zanzui kimenufaika kwa kupata kiasi cha Tshs. 7,674,545. 54  kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Vyumba 2 vya Madarasa, Choo matundu sita (6) na Ofisi ya Walimu moja (1).

Akizungumza na wananchi katika mkutano mkuu wa Kijiji cha Mwabujiku uliofanyika leo tarehe 20 April 2022 wenye lengo la kuhamasisha wananchi kujitolea nguvu kazi katika mradi huo, Afisa Ufuatiliaji   TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg John Wambura amempongeza Mh. Diwani kwa kuupigania huo mradi na amewaomba wananchi kujituma zaidi kwa sababu bado wapo nyuma. Na lengo la TASAF ni kuona mradi unakamilika kwa wakati .

Pia Afisa huyo ameongeza kuwa kuanzia tarehe 27 April 2022 kutakuwa na mafunzo ya siku tatu 3 katika Kata ya Zanzui ambayo yatahusisha wajumbe wa  kamati ya CMC kutoka Mwabayanda na Zanzui yenye lengo la kuweka mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.

Aidha Wambura amewasihi wanakamati wa CMC wasiwe na tamaa katika fedha hizo wawe waaminifu na wawazi ili mradi huo ukamilike kwa ubora unaotakiwa na amemuomba Mhe. Diwani kufuatilia kwa karibu utekelezaji huo kwenye suala la fedha.

Awali akiwasilisha taarifa Afisa Maendeleo ya Jamii Ndg.  Berther Lugenji amewaomba wananchi kutoa ushirikiano mkubwa wa nguvu kazi ili mradi ukamilike na fedha hizo zisiweze kuhamishwa na kupelekwa sehemu nyingine  kwa sababu serikali imetoa asilimia 90% kwenye mradi huo na wananchi wanatakiwa kuchangia asilimia 10% katika mradi huo kama ambavyo mlivyokubaliana katika kikao Cha mwanzo .

Kwa upande wake Ndg. Donatus Weginah Afisa Mipango wa Mkoa wa Simiyu ameelezea jinsi ambavyo wananchi wenyewe waliibua miradi hiyo kutokana na mahitaji waliyokuwa nayo na serikali imetimiza wajibu wake wa kutoa fedha ili kusaidia utekelezaji wa mradi huo na amewaomba wananchi kujitoa kama makubaliano yalivyokuwa.

"Wajibu wa msingi ni upatikanaji wa vifaa vya ujenzi ambavyo vipo katika maeneo yetu vifaa hivyo ni mchanga, kokoto, mawe, maji pamoja na nguvu kazi ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa muda uliopangwa” amesema Donatus

Aidha Diwani wa kata ya Zanzui Mh. Jeremia Mange Shigala ameishukuru Serikali ya Rais Samia Suluhu Hasan kwa kuwaletea fedha katika Kijiji Cha Mwabujiku kupitia mfuko wa TASAF ili wapunguze changamoto hizo za madarasa na vyoo katika Kijiji hicho na amewaomba Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji kutoa ushirikiano kwa wananchi katika zoezi hilo ili mradi ukamilike kwa wakati na waweze kuletewa miradi mingine.

Kwa upande wao wananchi wameupokea mradi huo na wameahidi kushiriki kikamilifu katika kazi hiyo na tayari wamepeleka mchanga katika eneo ambalo mradi utafanyika tayari kwa utekelezaji ili kuwasaidia watoto wao kupata mazingira mazuri ya kusomea.

Nae Mwalimu Mkuu wa Shule ya  Mwabujiku Mwl. Mariam Ngowi ameishukuru TASAF kwa kupeleka mradi huo katika shule yake  wa madarasa hayo mawili , choo matundu sita (6) na ofisi ya walimu itawasaidia kupunguza changamoto zilizopo hapo shuleni kwa sababu Madarasa waliyonayo Sasa hivi hayatoshelezi mahitaji ya wanafunzi katika shule hiyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.