• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

TAPSHA MASWA YAPATA VIONGOZI WAPYA

Posted on: November 6th, 2024


Umoja wa Walimu Wakuu Wilaya ya Maswa wamefanya uchaguzi na kupata viongozi wapya ambao wataongoza Umoja huo  kwa muda wa miaka mitano kwa mujibu wa kanuni za umoja huo.

Lengo la chombo hicho ni kuhakikisha kinasimamia taaluma na kushirikiana na ofisi ya mkuu wa divisheni ya elimu ya awali na elimu msingi wilaya kwa ajili ya kukuza taaluma.

Nafasi zilizokuwa zinagombewa ni Mwenyekiti wa TAPSHA Wilaya ya Maswa, Mwenyekiti Msaidizi, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi na Mhasibu wa TAPSHA Wilaya ya Maswa ambapo katika uchaguzi huo nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu walipita bila kupingwa kwa kuwa hapakuwa na wagombea zaidi ya wawili.

Katika Uchaguzi huo  Mwl. Mbaga Shilla amechaguliwa kwa awamu nyingine kuongoza umoja huo wa walimu wakuu Wilaya ya Maswa, ambapo nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa TAPSHA ni Mwalimu Florence Mwita, Katibu Mkuu wa TAPSHA Wilaya ni Lucas Zitto na Mhasibu wa TAPSHA Wilaya  ni Nyanswi Samwel.

Nafasi iliyopigiwa kura ilikuwa ni nafasi ya mhasibu ambapo kulikuwa na wagombea wawili ambao ni Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Nyalikungu Mwalimu Nyanswi Samwel na Mwalimu mkuu shule ya msingi Ngongwa Mwl Advera Charles.

Katika kinyang’anyilo hicho wapiga kura walikuwa 98 na Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Nyalikungu aliibuka kidedea kwa kupata kura 64 dhidi ya mpinzani wake aliyepata kura 34 na kutangazwa na Mwenyekiti wa Uchaguzi kuwa Mhasibu wa TAPSHA Wilaya ya Maswa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa TAPSHA Mkoa Mwl. Marco Manyenye amesema katika nafasi ya Katibu Msaidizi mgombea alipungukiwa sifa kwa mujibu wa kanuni za TAPSHA.

Baada ya ushindi huo viongozi hao wamewashukuru viongozi wenzao kwa kuwaamini na kuwachagua ili waweze kuwaongoza na pia wameahidi kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano umoja na kushauriana ili kujenga TAPSHA yenye nguvu na kuinua taaluma mashuleni.

Aidha Mwenyekiti wa TAPSHA Wilaya ya Maswa  baada ya kuchaguliwa amesema  Umoja na ushirikano ndio utakaoufanya umoja huo kufanya kile ambacho kimekusudiwa ili kuleta tija katika taaluma.

Akimwakilisha mlezi wa TAPSHA Wilaya ya Maswa ambaye pia ni Afisa Elimu msingi Wilaya ya Maswa, Afisa Taaluma Wilaya ndugu Joseph Omahe amewapongeza viongozi kwa kupata nafasi hiyo na amewaomba viongozi wa TAPSHA kuongeza kipengele kwa mgombea wa nafasi yeyote katika Umoja huo ahakikishe shule yake inafanya vizuri kitaaluma.

Pia ametoa wito kwa viongozi hao kusimamia taaluma na sio kuangalia maslahi yao binafsi bali wawe viongozi ambao watasimamia taaluma ya watoto ambao hawajajitambua.

Awali  katibu wa TAPSHA  Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Mwalimu mkuu shule ya Sangaitinje Wilaya ya Meatu  amewapongeza Walimu Wakuu kwa kuitikia wito wa kuchagua viongozi ambao watasukuma gurudumu la TAPSHA  kwa muda wa miaka mitano mingine kwa mujibu wa katiba.

Pia amesema TAPSHA ndio sauti ya Walimu Wakuu kwa kuisaidia serikali na kuisaidia Ofisi ya Afisa Elimu Msingi kuhakikisha kwamba wanasonga mbele kitaaluma.

"Niwaombe viongozi wenzangu kwa zoezi ambalo liko mbele yetu wapo viongozi ambao wamemaliza muda wao tumeona utendaji wao wa kazi tunakwenda kuchagua viongozi wengine tusichague viongozi kwa mhemuko, tusichague viongozi kwa kuangalia kwamba flani kafanya nini bali tuangalie atatufikisha wapi kwa upande wa taaluma"

Pia amesema viongozi hao wakiitumia vizuri TAPSHA itawasaidia kujifunza kwa majirani, wao kwa wao namna bora ya ufundishaji na hata wengine wanafanyaje kupata matokeo mazuri, pamoja na kutatua changamoto zinazowahusu wao.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.