Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani kimkoa imefanyika Wilayani Itilima mkoa wa Simiyu chini ya kauli mbiu "Kuunganishwa kwa Mifuko ya Hifadhafi ya Jamii kulenga kuboresha mafao ya wafanyakazi".
Mgeni rasmi ya siku ya leo katika sikukuu hii alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka. Katika hotuba yake ameahidi kutoa zawadi za kutambua vipaji vya watu wa Simiyu, ameahidi kumtambua Mwalimu mstaafu Mwl. Thomas mtunzi wa wimbo wa "acha nilingie kazi yangu ya ualimu", wimbo unaotumika kwenye matamasha ya Walimu Mkoani Simiyu siku zote.
Pia amerejea hotuba yake ya mei mosi 2017 pale Lamadi wilayani Busega aliyowataka viongozi kubadilika na matokeo yake yanaonekana.
Amewaasa watumishi wajipange na kuandaa mazingira yao mazuri ya baadaye baada ya kustaafu kwa kujenga nyumba zao mapema kabla ya kustaafu ili waishi vizuri.
Amewahimiza walimu kutumia fursa zilizopo kwa kuwaambia kufundisha tution wakati wa likizo ili kuwaweka wanafunzi wetu katika hali ya kuelewa. Muda wote watoto wapishane wakiwa na vitabu na madaftari ili kuinua kiwango cha elimu kuliko kukutana nao wakiwa na mifugo.
Amesema kuwa anajivunia wananchi wa Simiyu kwani wanafanya kazi kwa nguvu na Watumishi wanafanya kazi kwa moyo. Amewapongeza wafanya kazi wa Mkoa wa Simiyu kwa juhudi zao za kuleta mabadiliko.
Amewajulisha wananchi wote wa Mkoa wa Simiyu kuwa Mkoa umepata fedha kwa ajili ya kujenga shule 3 za kisasa.
Amewakumbusha watumishi kuipenda kazi yao na Mkoa wetu kwa ujumla ili kuleta chachu ya maendeleo na mafanikio.
Sherehe zimehudhuriwa na Watumishi mbalimbali kutoka kila Wilaya wakiongozana na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wakuu wa Idara na Vitengo. Aidha watumishi mbalimbali kutoka kila kada wametunukiwa zawadi za vyeti, fedha na vifaa vingine vilivyokabidhiwa na Mgeni rasmi.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.