• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Shilingi Milioni 519 kutatua changamoto ya maji kijiji Cha Mwashegeshi

Posted on: December 4th, 2023

Kijiji Cha Mwashegeshi kilichopo kata ya Nguliguli ni miongoni mwa vijiji vilivyokuwa na ukosemu wa huduma ya maji safi na salama  hivyo kupelekea wananchi wake kutumia maji yasiyo salama na Safi kutokana na changamoto hiyo serikali iliiona adha hiyo na kutoa kiasi Cha shilingi milioni 519 kwa ajili ya kupeleka mradi wa maji katika Kijiji hicho.

Lengo la serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama pamoja  na kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayotokana na utumiaji wa maji yasiyo salama na pia kutunza chanzo Cha maji ambacho kinasamabaza maji katika mji wa Maswa na vijijini 11.

Kamati ya siasa Wilaya ya Maswa ilifika katika mradi huo kukagua na kuona namna utekelezaji unavyoendelea ambapo wajumbe wa kamati hiyo walitoa  pongezi  kwa Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi milioni 519 kwa ajili ya kutatua changamoto ya maji katika Kijiji Cha Mwashegeshi

“Nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mhe Rais Mama yetu Dkt Samia Suluhu Hassan kwa nia yake na dhamira ya dhati ya kumtua mama ndoo kichwani kwa mradi huu wa maji katika kijiji hiki cha mwashegeshi wenye thamani ya milioni 519 tunapata mradi huu katika kijiji hiki ambao unakwenda kutatua kabisatatizo la upatikanaji wa maji”. Mwenyekiti wa CCM Wilaya

Akizungumza katika ziara hiyo ya  utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika eneo la mradi wa tenki la maji  ambalo litasambaza maji katika Kijiji hicho Mwenyekiti wa CCM Wilaya Mhe Onesmo Makota alisema mradi huo ni mkubwa hivyo amewataka wananchi kuutunza ili udumu kwa muda mrefu

Nae Diwani wa Kata ya Nguliguli Mhe Peter Mathias alimpongeza Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa Fedha kiasi Cha shilingi milioni 519 kwa ajili ya kutatua kero hiyo ambayo ilikuwepo miaka 30 sambamba na hilo pia alitoa pongezi kwa Wabunge wote na  Mhe Mkuu wa Wilaya kwa usimamizi na ufatiliaji wa mradi huo mpaka ukaanza.

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge alitoa shukrani kwa serikali ya awamu ya sita kwa kutoa Fedha nyingi katika wilaya ya Maswa hususani katika miradi ya maji ambayo inatekelezwa ili ifikapo mwaka 2025 wananchi wawe wamepata maji kwa asilimia 95 mjini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya majisafi na Usafi wa Mazingira Maswa (MAUWASA) Mhandisi Nandi Mathias alibainisha shughuli mbalimbali ambazo zinatekelezwa katika mradi huo ikiwepo ujenzi wa tenki kubwa lenye ujazo wa Lita  laki moja na  ulazaji wa bomba kilometa 11.

Aidha aliongeza kuwa katika kuhakikisha bwawa hilo linahifadhiwa Mamlaka hiyo inajenga mbauti kwa ajili ya kunyweshea ng'ombe pamoja na ujenzi wa vituo 6 vya kuchotea maji ambapo mpaka sasa kazi hiyo inaendelea ambapo ikikamilika itanufaisha wananchi wengi.

Mjumbe wa kamati ya siasa Wilaya Ndg Mwashi Shidile alimshuru Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwatua akina mama ndoo kichwani kwa sababu wana majukumu mengi majumbani mwao hivyo ujio wa mradi huo utawasaidia sana.

Wakiwa katika ziara hiyo kamati ya siasa Wilaya ya Maswa ilikagua  miradi 12 ya Elimu, Afya, maji, barabara pamoja na umeme ambapo kamati hiyo imeridhishwa na miradi yote hiyo  na kuomba miradi ambayo haijakamilika ikamilike kwa wakati kutokana na mkataba ulivyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.