• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC awataka wananchi kuchangamkia fursa za zana za kilimo

Posted on: July 5th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt Yahaya Nawanda amewataka wananchi wa Maswa na wilaya jirani kuchangamkia fursa za zana za kilimo ambazo zitawasaidia katika shughuli mbalimbali za kilimo na ufugaji.

Dkt Nawanda amesema hayo akiwa katika kituo cha zana za kilimo na teknolojia vijijini (CAMERTEC) kilichopo kijiji cha Mwandete Kata ya Sangamwalugesha wakati akitembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Mkuu wa mkoa amesema kuwa wananchi wa Maswa wanatakiwa wafike katika kituo hicho ili kupata mafunzo ya teknolojia mpya, ushauri na kukodi zana hizo ili ziwasaidie katika kujiongezea kipato.

Pia Mkuu wa Mkoa amewataka wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuwapeleka vijana wanaojishughulisha na kilimo kufika katika kituo hicho cha zana za kilimo ili waweze kujifunza mbinu bora za kutumia teknolojia mpya ya zana za kilimo zitakazowasaidia kulima kwa tija ili kupata mazao mengi.

Kwa upande wake Mhe. Diwani wa Kata ya Sangamwalugesha amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupeleka kituo hicho katika Kata yake kwa kuwa kimekuwa msaada mkubwa katika eneo lake kwa wakulima na wafugaji pia amewataka wananchi kutoka Kata zingine kufika katika kituo hicho ili kupata ujuzi kuhusu zana hizo za kilimo.

Kituo hicho kinatoa huduma mbalimbali zikiwepo mashine za kupura mazao mbalimbali kama vile Mahindi, Mtama, Karanga na Alizeti, huduma ya uwekaji wa vifaa vya gesi asilia inayotokana na kinyesi cha wanyama, matela ya kubebea mizigo, mashine za kupandia mazao na mashine za kukatia viazi (michembe).

Akiwa Wilayani Maswa Mkuu wa Mkoa ametembelea kikundi cha vijana Maswa Diagnostic Centre kilichopo Shanwa kinachojishughulisha na utoaji wa huduma ya upimaji ambacho kilipata mkopo wa shilingi milioni 16 ya asilimia 10 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa ajili ya kutoa huduma ya vipimo vya magonjwa mbalimbali ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali na vituo vya afya.

Aidha ametembelea kiwanda cha mjasiriamali Liliani Kinyemi (ABC) ambacho kinashirikiana na Halmashauri kwa ajili ya kuongeza virutubishi kwenye unga wa mahindi, mchele na ulezi kwa kuongeza virutubishi aina ya zinki, chuma, foliki asidi na vitamin B12 ambavyo vitawasaidia watoto wanaozaliwa kuzuia utapiamlo na kupunguza udumavu katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Pia amekagua tenki la maji katika Kata ya Nyalikungu lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni moja, ujenzi wa shule mpya ya msingi katika Kata ya Jija, ujenzi wa shule mpya ya msingi katika Kata ya Shishiyu na kituo cha afya Badi.

Dkt Nawanda amempongeza Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha nyingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa ajili ya ujenzi wa shule za msingi mpya, vituo vya afya, matenki ya  maji na barabara.

Kwa upande wa wananchi wamemshukuru Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutoa Fedha ambazo zimewezesha kujenga miundombinu mbalimbali yenye lengo la kuwasaidia wananchi kupata huduma hizo kwa uhakika ikiwepo vituo vya Afya, Shule na Maji.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.