• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC asisitiza viongozi kusimamia Usafi wa Mazingira katika maeneo ya makazi ya wananchi

Posted on: January 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt Yahaya Nawanda amewataka viongozi wote kuanzia ngazi ya Wilaya mpaka Kijiji kuhakikisha wanahamasisha Usafi wa Mazingira katika maeneo yote ya kazi na makazi ili kuepukana na ugonjwa wa kuhara na kutapika.

Dkt Nawanda ametoa agizo hilo katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na kuhudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa, mganga mkuu wa Mkoa, mkuu wa Wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya, kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Maswa, wakuu wa Divisheni, kamati ya CHMT ya Wilaya, Maafisa Tarafa, watendaji wa Kata na vijiji, wazee maarufu na viongozi wa dini.

"Viongozi wa dini pamoja na wazee maarufu Mimi nawaombeni sana Kila mmoja katika eneo lake aende akahamasishe Usafi wa Mazingira. Mimi ninaamini viongozi wa dini pamoja na ninyi wazee mkisema huu ugonjwa basi hapa Maswa hakuna mtu atakayehara Wala kutapika Mimi nimekuja hapa kuhamasisha Usafi wa Mazingira." Amesema Dkt Nawanda

Mkuu wa Mkoa amepiga marufuku wananchi kula chakula katika mikusanyiko ya watu kama vile msibani, pia ametoa wito maeneo yote ya migahawa yanatakiwa kuwa na maji ya kuchemshwa yaliyowekwa kwenye ndoo, sambamba na hilo ametoa zuio kwa wafanyabiashara wa mahindi ya kucheshwa kuuzwa maeneo ya  stendi.

"Sehemu zote za kuuza pombe za kienyeji zisizo na vyoo zote ni marufuku na mpige fullstop kuanzia Leo hii kwa sababu ya mtu akilewa hachagui sehemu ya kwenda haja." Amesema Dkt  Nawanda

Aidha amewataka viongozi wa MAUWASA na RUWASA kutoa huduma ya  maji bure katika maeneo yote yaliyoathirika na tatizo la kuhara na kutapika kwa kipindi Cha mwezi mmoja na kutibu maji hayo kwa kutumia dawa katika visima vilivyochimbwa na wananchi binafsi ili wananchi wasiwe na kisingizio cha kutokupata maji safi na salama.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amesema baada ya kupata taarifa  27 Disemba 2023 kuwa Kuna ugonjwa wa kuhara na kutapika  timu za ufatiliaji ziliundwa lengo likiwa ni kutoa elimu na  kuhakikisha wananchi wanakuwa na vyoo bora na wanavitumia .

"Kwa ambao hawana vyoo tulisisitiza timu hizo kuanzia ngazi ya Wilaya, Kata na Kijiji kutoa elimu kwa wananchi pale ambapo imeshindikana watu hawajatii elimu na kuzingatia basi hatua za kisheria zichukuliwe kwa wananchi hao. Na tayari hatua hizo zimeanza kuchukuliwa."amesema Mhe Kaminyoge

"Tumefanya jitihada kubwa kwa kushirikiana na Maafisa kutoka Wizara ya Afya wapo  lakini tumepata ushirikiano mkubwa  wa Maafisa kutoka ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wetu wakiongozwa na Mganga Mkuu wa Wilaya Kila siku tunao kwa ajili ya kuhakikisha kwamba ugonjwa wa kuharisha tunautokomeza na usiendelee kuathiri wananchi wetu." Amesema Mhe Kaminyoge

Pia Mkuu wa Wilaya amesema mikakati imewekwa ambapo suala kubwa ilikuwa ni kuwaelimisha na kuwasisitiza wananchi kufata kanuni za afya kupitia  kamati ya afya ya wilaya.

Mkuu wa Mkoa akiwa wilayani Maswa amekagua kaya 12 katika Kata ya Shanwa ili kuona Usafi wa Mazingira ulivyo katika maeneo hayo hasahasa vyoo wanavyovitumia wananchi katika kaya zao na maeneo ya biashara.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.