• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC aipongeza Maswa kwa kupata hati safi

Posted on: June 20th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt Yahaya Nawanda ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu za serikali

Dkt Nawanda amesema hayo katika kikao Cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa leo tarehe 20.06.2023 kilichokuwa na ajenda ya kujadili hoja ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG).

Mkuu wa Mkoa amesema hoja zote zilikuwa 98 ambapo hoja 66 zimepata majibu na 32 zinaendelea kutekelezwa ili zifungwe.

"Nichukue nafasi hii kumpongeza CAG kwa kazi nzuri anayoifanya kwa hakika amefanya kazi nzuri sana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itaendelea kushirikiana na wewe" amesema Dkt Nawanda.

Pia Mkuu wa Mkoa amewasisitiza wakuu wa Idara kusimamia vizuri majukumu yao ili kuepuka kuzalisha hoja mpya, sambamba na hilo pia amemwagiza mkuu wa Kitengo cha Fedha kuwasisitiza wakusanya  Mapato kupeleka Fedha benki mara baada ya kukusanya fedha hizo ili kuepuka watumishi hao kupoteza mapato ya Halmashauri na wao kuingia katika matatizo  ambayo yatawasababishia shida katika utumishi wao.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Ndg Prisca Kayombo amewashukuru viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa ushirikiano waliouonesha kwa kuwezesha ripoti ya mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali kutekeleza hoja zote  kwa asilimia 100%.

Pia Ndg Kayombo amewaomba waheshimiwa madiwani na wataalamu kuendelea kufanya kazi zaidi ili kuitoa Maswa mahali ilipo na kuifikisha sehemu nzuri ili kuweka rekodi nzuri.

Nae Mwenyekiti wa Chama Cha mapinduzi wilaya ya Maswa Mhe. Onesmo Makota amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuleta Fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo Katika wilaya ya Maswa.

" Kwa niaba ya Chama Cha Cha Mapinduzi wilaya nikupongeze wewe kwa namna ambayo unachapa kazi hotuba yako Mkuu wa Mkoa imegusa maeneo yote kwenye kuelekeza , kuonya, kushauri hongera sana". Amesema Makota

Aidha Mhe. Makota amewapongeza watendaji wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa pamoja na  waheshimiwa Madiwani kwà kupata hati safi ambayo imezalishwa na utendaji mzuri wa watumishi hao katika kutimiza majukumu yao  kwa kila mtu katika eneo lake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Maswa Mhe. Paul maige amesema umoja na mshikamano ndio utaimalisha  mapato  katika Halmashauri ya Maswa  na kuondoa hoja ambazo zinapatikana katika Halmashauri na kutimiza matakwa ya kisheria.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.