• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC achangia mifuko Hamsini ujenzi wa choo

Posted on: December 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt Yahaya Nawanda amechangia mifuko 50 ya simenti kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyoo katika shule ya sekondari Malampaka ambayo majengo yake yamejengwa kwa ubora zaidi ya majengo mengine.

Nawanda amesema wilaya ya Maswa imepewa zaidi ya shilingi bilioni 30   na serikali ya Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani kwa ajili ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya ya Maswa ikiwa bilioni 3 zimeletwa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ambayo itakuwa na mabweni.

Amesema hayo katika stendi ya Malampaka wakati akizungumza na wananchi wa Malampaka na kusikiliza kero zao na kuwaeleza wananchi miradi mbalimbali inayotekelezwa na ambayo imetekelezwa katika wilaya ya Maswa ikiwepo mradi wa reli ya kisasa ambapo makao makuu yatakuwa Malampaka hivyo itakuza uchumi na kuongeza mapato ya Wilaya pamoja na mwananchi mmojammoja.

Dkt Nawanda amesema zao la pamba ni muhimu sana na Mkoa wa Simiyu unatakiwa kuzalisha Tani 300,000 za pamba kwa mwaka huu hivyo amempongeza balozi wa pamba Tanzania Mhe Agrrey Mwanri ambaye yupo wilaya ya Maswa kwa kutoa Elimu nzuri ambayo wakulima wa pamba wanatakiwa kufata kwa kuwa katika Mkoa wa Simiyu Tani 500,000 zinatakiwa kuzalishwa ifikapo 2025.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema balozi wa pamba amesaidia kutoa Elimu nzuri kwa wakulima ambayo itawasaidia  kutumia vipimo vya sm.60  kwa kila mstari na sm.30 kwa kila mche, kuchoma mabaki yote ya pamba ya msimu uliopita, na kuwataka maafisa ugani wote kuwa na shamba ili iwe mfano mzuri kwa wakulima wote kujifunza kwao.

Pia Mkuu wa mkoa amewasisitiza wananchi kuwaamdikisha watoto wote wenye umri wa kuanza shule kwa Elimu ya awali na msingi muhula wa 2023 waandikishwe ili kujua idadi ya watoto hao katika Wilaya ya Maswa na Mkoa mzima wa Simiyu pia amewataka wananchi wote kuchangia chakula shuleni ili ufaulu wa wanafunzi uongezeke.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya amempongeza Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kuleta zaidi ya shilingi bilioni 35 ya miradi mbalimbali ikiwepo Zahanati, Vituo vya Afya, Barabara, Umeme na Maji.

Mkuu wa Mkoa yupo Maswa kwa ziara ya siku tatu kutembelea miradi katika Tarafa tatu na ameambatana na viongozi mbalimbali wa Mkoa, wakuu wote wa taasisi, wakuu wa idara, kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Maswa.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO March 02, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rc ataka ushirikiano kwa wanawake Simiyu uendelee

    March 09, 2023
  • Walimu Wakuu, Maafisa Elimu Kata na Wenyeviti wa Kamati wapata mafunzo

    March 06, 2023
  • MUAC kutambua watoto wenye matatizo ya lishe

    March 04, 2023
  • DC asisitiza wakulima wote wapatiwe mabomba

    March 03, 2023
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS
  • Mfumo wa MVC-MIS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.