• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mwenge wa Uhuru waridhishwa na miradi ya maendeleo Maswa

Posted on: July 27th, 2023

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Abdalla Shaib Kaim ameipongeza Wilaya ya Maswa iliyopo Mkoa wa Simiyu kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo kwa sababu Mwenge wa Uhuru umepita katika miradi hiyo  na kuridhishwa nayo kwa kuwa imetekelezwa  kwa ufanisi na weredi.

Akiwa wilayani Maswa Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa amezindua jengo la Wagonjwa wa nje, mama na mtoto, katika Zahanati ya Nguliguli katika Kata ya Lalago ambapo mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 271 ambazo zimetolewa na serikali kupitia mfuko wa global fund.  

Zahanati hiyo itakuwa na uwezo wa kuhudumia wananchi 17,079 ambao walikuwa wakitembea umbali mrefu kutatafuta huduma hiyo sambamba na hilo, pia amegawa vyandarua kwa makundi maalumu ambayo ni mama wajawazito wazee na watoto chini ya miaka mitano.

Aidha Ndg Kaim ameweka jiwe la msingi ujenzi wa Bweni la wasichana katika shule ya sekondari Mwagala lililopo Kata ya Lalago lenye thamani ya Shilingi milioni 114 ambapo Fedha hizo zimetolewa na serikali kupitia mradi wa  EP4R, Halmashauri ya Wilaya ya Maswa pamoja na nguvu za wananchi ambapo ujenzi wake upo katika hatua za ukamilishaji.

Pia kiongozi wa Mwenge wa uhuru amepanda mti katika bweni hilo, kuzindua klabu ya wapinga rushwa na kutoa cheti katika shule ya sekondari Mwagala, kukagua na kuona utoaji wa Elimu ya lishe inayozingatia makundi matano ya vyakula kwa njia ya kupika vyakula vyenye lishe bora.

Katika hatua nyingine Ndg. Kaim amezindua mradi wa tenki la kuhifadhi  maji lenye ujazo wa Lita milioni moja na mfumo wa usambazaji maji katika Kata ya Nyalikungu wenye thamani ya bilioni 1 tenki hilo ambalo litasambaza maji katika vitongoji 25 kati ya 40 vya mji wa Maswa na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa Wilaya ya Maswa.

Vilevile kiongozi wa Mwenge wa Uhuru kitaifa ametembelea na kuona vifaa tiba vinavyotumika katika shughuli za kimaabara katika kikundi cha vijana kilichopo katika Kitongoji cha Kumalija Kata ya Shanwa, kikundi hicho kimeanzisha Maabara yenye thamani ya shilingi milioni 18 ambayo wamewezeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa kupatiwa kiasi Cha shilingi milioni 16 kutoka asilimia 10  na wao kutoa kiasi cha shilingi milioni mbili kwa ajili ya kutoa huduma ya vipimo vya magonjwa mbalimbali ili kupunguza msongamano katika vituo vingine vya kutolea huduma za Afya.

Mradi ambao utawasaidia vijana kiuchumi kwa kujiajiri na kuajiri wengine kwa lengo la kujipatia kipato na kusogeza huduma karibu kwa wananchi ambapo vipimo vinavyotolewa hapo ni upimaji wa   tezi dume na vipimo vingine vingi.

Ndg. Kaim amewapongeza vijana hao kwa kuwa na moyo wa kizalendo  ubunifu na weredi kwa kufanya jambo hilo ambalo limewavutia pia amewapa kongole Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa kuwawezesha vijana hao Fedha ya mkopo wa asilimia 10 ili waweze kujiajiri wenyewe.

Pia kiongozi wa Mwenge wa Uhuru kiatifa ametembelea na kuona utoaji wa Elimu katika kupambana na maabukizi ya VVU- UKIMWI na kuona namna Elimu inavyotolewa pamoja na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.