• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Miradi ya Boost kuboresha mazingira ya ufundishaji Maswa

Posted on: October 19th, 2023

Mradi wa BOOST ni mradi ambao upo kwa ajili ya kuinua elimu ya  Awali na  Msingi, lengo kuu la mradi huu ni kuboresha upatikanaji wa fursa katika ufundishaji na ujifunzaji bora wa elimu ya awali na msingi katika ujenzi wa miundombinu ya elimu.

Kutokana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika sekta ya elimu hasahasa elimu ya msingi kuwa na uhaba wa madarasa ambapo inapelekea wanafunzi zaidi ya 200 au 150 kukaa darasa moja, upungufu wa vyoo  na shule za Watoto wa chekechea, serikali ya awamu ya sita iliona changamoto hizo na kuja na mwarobaini wa kutatua changamoto hizo katika maeneo husika.

Halmashauri ya wilaya ya Maswa ni miongoni mwa Halmashauri zilizonufaika na mradi huo ambapo serikali ya awamu ya sita chini ya Rais shupavu  Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ilitoa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kupitia mradi wa BOOST kwa ajili ya kutatua changamoto na kuboresha miundombinu mbalimbali ikiwepo ujenzi wa shule mpya 3, ujenzi wa matundu ya vyoo na ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw. Maisha S. Mtipa ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya Maswa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya  kuboresha  miundombinu katika idara ya elimu hasa upande wa elimu ya msingi.

Bw. Mtipa aliogeza kuwa fedha hizo zimejenga miundombinu mbalimbali katika majimbo yote mawili ya Maswa ambapo katika jimbo la Maswa Magharibi  kiasi cha shilingi bilioni 1.014,200,200/= zimetumika kujenga shule mbili mpya za msingi na madarasa ya mfano ya chekechea ambapo shule moja ni ya mikondo miwili iliyopo Kijiji cha Jija Kata ya Jija,ujenzi wa shule mpya ya msingi Majengo yenye mkondo mmoja iliyopo Kijiji cha Shishiyu kata ya Shishiyu ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu ya vyoo 3 katika shule ya msingi Igunya iliyopo Kata ya Jija pamoja na ujenzi wa madarasa ya mfano ya chekechea katika shule ya msingi Mwabayanda Kata ya Mwabayanda.

Kwa upande wa Maswa Mashariki kiasi cha shilingi milioni 567,400,000/= zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Mwakabeya yenye mkondo mmoja, ujenzi wa vyumba vya madarasa  3 na matundu matatu ya vyoo katika shule ya msingi Ipililo B, ujenzi wa vyumba vya madarasa vitatu na matundu ya vyoo katika shule ya msingi Ngudu iliyopo Kata ya Bugarama, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu 3 ya vyoo katika shule ya msingi Nguliguli iliyopo Kata ya Nguliguli.

“Fedha hizi zote shilingi bilioni 1,581,600,000/= zimepelekwa kuboresha miundombinu mbalimbali na ujenzi wa shule mpya kabisa za kisasa ambappo kwa mazingira hayo imeweza kupunguza adha kubwa ya msongamano wa wanafunzi katika maeneo mbalimbali, imeboresha  miundombinu kwa hiyo mazingira ya ufundishaji kwa sasa yamekuwa  bora kabisa  na changamoto zote za ufundishaji zitakuwa zimeisha” Alisema Mkurugenzi Mtendaji.

Kwa upande wa walimu wakuu waliopata fursa ya mradi huo wamemshukuru Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fedha hizo za ujenzi wa miundombinu hiyo ya elimu  kwa sababu  ametatua changamoto katika shule hizo ambazo wanafunzi walikuwa wanatembea umbali mrefu kutafuta elimu, pia kulikuwa na msongamano mkubwa wa wanafunzi katika darasa moja hivyo ujio wa shule  hizo utaboresha mazingira ya ufundishaji na watoto wa chekechea wataweza kusoma vizuri na kwa kuzingatia umri wa kuanza masomo hayo.

Nao watendaji wa  Kata wamemshukuru Mhe Samia Suluhu Hassan kwa miradi hiyo ambayo itasaidia wanafunzi kutatua kero mbalimbali za wanafunzi kwa  kupunguza msongamano wa wanafunzi katika darasa moja sambamba na hilo wamemuahidi Mhe Rais kuwa miradi hiyo watailinda na kuisimamia vizuri ili idumu kwa muda mrefu.

Wanafunzi wa shule mbalimbali zilizonufaika na mradi huo wamemshukuru Mhe  Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea miundombinu hiyo ya madarasa, vyoo na shule hizo mpya ambapo itasaidia kutatua changamoto ya kukaa dawati moja wanafunzi watano au wanne, pia wamesema vyoo hivyo vitasaidia kuokoa muda wa masomo maana kabla ya mradi huo vyoo vilikuwa vichache hivyo kupoteza muda mwingi wa masomo na wameahidi kusoma kwa bidii ili wawe viongozi wakubwa wa baadae katika taifa hili.

Kwa nyakati tofauti wananchi nao hawakuwa nyuma kumpa kongole Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa miradi hiyo kwa sababu wananchi hawajachangia fedha yoyote wala nguvu kazi katika miradi hiyo na pia wameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa kuwaona na kupeleka miradi hiyo katika maeneo yao ambapo kwa kiasi kikubwa itasaidia Watoto wao kusoma katika mazingira mazuri.

Majengo ya vyumba vya madarasa katika Shule Mpya ya Msingi Majengo iliyoko Shishiyu

Majengo ya vyumba vya Madarasa katika Shule ya Msingi Mwakabeya

Muonekano wa madarasa ya Awali katika Shule ya Mwabayanda

Muonekano wa Shule ya Awali ya Majengo iliyoko Shishiyu

Vyumba 2 vya Madarasa katika Shule ya Msingi Igunya

Vyumba 2 vya Madarasa katika Shule ya Msingi Nguliguli


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.