• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Wilayani Maswa

Posted on: May 22nd, 2019

Mwenge wa uhuru Wilayani Maswa umepokelewa kwa furaha nderemo na vifijo katika kijiji cha Jihu Kata ya Badi ukitokea Wilaya ya Kwimba Mkoa wa Mwanza.

Ulikabidhiwa Wilayani Maswa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu kuupokea kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na baadaye kumkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Maswa.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2019, Mzee Mkongea Ali pamoja na timu yake wameridhia miradi yote mwenge uliyopitia kama ilivyopendekezwa na uongozi wa Wilaya ya Maswa. Aidha Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa amefurahishwa na juhudi za wananchi kubuni miradi na hatimaye Serikali kuunga nguvu zao.


Mwenge wa Uhuru Wilayani Maswa umeweka jiwe la Msingi katika mradi wa Maji Jihu - Ikungu na kupanda miti katika eneo la chanzo cha maji hayo katika kijiji cha Nyashimba, Umetoa hati kwa Wananchi wa Mji wa Malampaka ikiwa ni hatua ya urasimishaji ardhi kwa Wananchi, Umeweka Jiwe la Msingi katika Kiwanda cha kusindika Viazi Lishe kilichopo Njiapanda Kata ya Isanga, Umetembelea, kuona na kukagua mradi wa barabara ya Lami yenye urefu wa Km. 1.5 mjini Maswa na umefungua Vyumba 2 vya Madarasa na ofisi 1 katika Shule ya Sekondari Sukuma.


Kiongozi wa mbio za Mwenge amekagua mabanda mbali mbali ambayo ni banda la TAKUKURU ambapo amezindua Klabu ya kupambana na rushwa ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Lalago, Banda la mapambano dhidi ya madawa ya Kulevya chini ya Klabu ya Wapinga madawa ya kulevya kutoka katika shule ya Sekondari Lalago, banda la uchaguzi lililokuwa linatoa elimu ya uchaguzi hasa maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za mitaa, banda la wajasiliamali mbali mbali (vikundi vya Vijana, akina Mama na Walemavu) wakiwa na bidhaa zao na banda la afya ambapo amegawa vyandarua kwa akina Mama wajawazito, Watu wenye ulemavu na akina Mama wenye watoto chini ya miaka 5. Aidha baada ya kukagua mabanda hayo alikabidhi hundi yenye thamani ya shilingi 6,800,000/= kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Walemavu.


Wananchi Wilayani Maswa wamejitokeza kwa wingi katika vijiji vyote Mwenge ulipopita huku wakishangilia katika makundi mbalimbali.


Baada ya kazi zote hizo shamrashamra ziko Lalago kisha kesho utakabidhiwa katika kijiji cha Sangaitinje  Wilaya ya Meatu.


Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 ni “Maji ni Haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa”.

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.