• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Matumizi sahihi ya Ardhi kunufaisha Maswa kiuchumi

Posted on: July 11th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge ameishukuru Serikali kwa kutoa Fedha kiasi cha shilingi bilioni 3 kwa ajili ya uboreshaji usalama wa milki za ardhi ili kutekeleza mpango wa matumizi ya ardhi, kuandaa matumizi sahihi ya vijiji kupitia mipaka mipya na kutoa hati miliki za kimila katika wilaya ya Maswa.

Mradi huo umepanga kuboresha usalama wa milki ya ardhi kwa kupanga, kupima, kusajili hati milki za kimila laki tano(500,000) ambapo wilaya ya Maswa inakusudiwa kunufaika na mradi huo kwa kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi ya vijiji 100 na kuandaa hati milki za kimila 100,000.

Mkuu wa Wilaya amesema hayo katika kikao Cha wadau katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakati wadau wakijadili mpango wa matumizi ya ardhi wilaya ya Maswa.

Mpango wa matumizi ya ardhi ya Wilaya umeainisha miradi mbalimbali inayopaswa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka 20 ijayo ili kutatua changamoto zilizoainishwa kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi wa Maswa.

Mhe. Kaminyoge amesema kutokana na ongezeko la watu mji umebadilika kuwa na migogoro ya ardhi, ukuaji wa makazi yasiyopangwa, upungufu wa huduma za jamii na uharibifu wa Mazingira ili kukabiliana na changamoto hizo wilaya haina budi kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi ambayo ni nyenzo ya upangaji inayoainisha matumizi mbalimbali ya rasilimali ardhi kulingana na hali halisi ya kiuchumi na kijamii.

Aidha mkuu wa Wilaya amesema utekelezaji wa mpango huo katika Halmashauri ya Maswa utaleta matokeo chanya katika kuchochea maendeleo ya Wilaya pamoja na kuleta usalama wa milki za ardhi, kukuza huduma za kijamii, kuboresha uhifadhi wa Mazingira na kumaliza migogoro inayotokana na ardhi.

"Naamini mpango huu ni mwarobaini wa matatizo ambayo waheshimiwa madiwani, waheshimiwa wabunge, Mkurugenzi Mtendaji, watendaji wa Kata na vijiji mnapambana nayo katika shughuli za kuwahudumia wananchi." Amesema Mkuu wa wilaya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Maisha Mtipa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta mradi huo wa uboreshaji wa usalama mradi ambao unaenda kutatua kero za mipaka, na migogoro ya matumizi ya ardhi.

Kwa upande wake meneja mradi wa urasimishaji vijijini Bw Joseph Onesmo  amesema serikali imetoa Fedha kiasi Cha shilingi US Dola milioni 150 ambayo ni sawa na shilingi bilioni 345 kutekeleza mradi huo katika wilaya Saba za Tanzania ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imepata kiasi Cha shilingi bilioni 3 kutekeleza mradi huo.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe. Paul  Maige amemshukuru Rais kwa kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi  kwa fursa waliyoipata ya mradi huo mkubwa ambao unatekelezwa katika Halmashauri Saba tu Tanzania nzima, pia amewaomba kila mmoja akasimamie na kushiriki kikamilifu katika mradi huo  ili kuhakikisha Halmashauri inazalisha kwa tija ili kuinua uchumi na kuchangia kwa asilimia kubwa katika ajira.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.