• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MAMLAKA YA MJI MDOGO MASWA YAVUJWA NA KULIDHIA AZIMIO LA KUANZISHWA HALMASHAURI MBILI

Posted on: February 17th, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa limeridhia azimio la kufuta Mamlaka ya mji mdogo wa Maswa na kuridhia azimio la kuanzisha kwa Halmashauri mbili za Maswa Mashariki na Maswa Magharibi ili kusogeza huduma kwa wananchi za kiuchumi, kisiasa na kijamii

Hayo yalisemwa na Waheshimiwa Madiwani katika kikao Cha baraza la Madiwani Cha robo ya pili ya mwaka wa Fedha 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Mamlaka ya mji mdogo Maswa ilianzishwa mwaka  2010 kufatia tangazo la serikali la GN NO: 287 la mwaka 1993 lengo likiwa ni kusimamia maendeleo ya shughuli za kiuchumi.kisiasa na kijamii,

Jukumu likiwa ni  kusimamia mpango wa bajeti matumizi ya kawaida, kudumisha mahusiano mazuri kati ya Mamlaka ya mji mdogo na Halmashauri ya Wilaya pamoja na kusimamia Usafi wa mji katika kaya, mitaa, vitongoji na sehemu za umma.

Tangu mwaka 2010 Hadi Sasa ni takribani miaka 13 Mamlaka ya mji mdogo wa Maswa umeshindwa kutekeleza majukumu yake kwa sababu ili Mamlaka ya mji mdogo iweze kuwa Halmashauri ya mji ni lazima iwe na eneo la Kata 12 lakini mpaka sasa Ina Kata 4 tu hivyo kutokizi vigezo hivyo.

Pia Mamlaka hiyo imeshindwa kusimamia vyanzo vya mapato na kuendelea kuipa mzigo Halmashauri ya Wilaya kwa kuendelea kulipa posho kwa watumishi wa Mamlaka ya mji mdogo sambamba na hilo pia kutokusimamia vizuri Usafi wa mji na kusababisha magonjwa ya mlipo.

Kutokana na mambo yote hayo Mamlaka ya mji mdogo tangu kuanzishwa kwake imeshindwa kufikia malengo ya kuanzishwa kwake kwa kutekeleza kwa ufanisi majukumu iliyokabidhiwa kwa Mamlaka hiyo hivyo baraza rikaridhia kufutwa Rasmi kwa mji huo na kuanzishwa Halmashauri mbili.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw. Maisha Mtipa alisema Madiwani kwa kauli moja wameridhia azimio la kuvunja Mamlaka ya mji mdogo kwa kuwa Mamlaka hiyo imekosa sifa kwa sababu imeanzishwa muda mrefu lakini Bado haijaweza kujitegemea.

Aidha Bw. Mtipa alisema Mamlaka hiyo imeendelea kuongeza mzigo kwa Halmashauri ya Wilaya kwa kuwa Halmashauri Ina Kata 36, vijiji 120, vitongoji 510 ambapo Mamlaka ya mji ilikuwa na vitongoji 40 lakini hawakuweza kufanikisha kuanzishwa kwa Halmashauri ya mji.

"Wajumbe wakaona afadhali ivunjwe kwa sababu inakosa sifa ya kuwa Halmashauri, pia wajumbe nao wamepitisha kwa kauli moja kuanzishwa kwa Halmashauri mbili kutokana na vigezo vya majimbo ambapo Jimbo la Maswa Mashariki lina Kata19  na Jimbo la Maswa Magharibi lina Kata 17  ili kusogeza huduma kwa jamii." Alisema Mkurugenzi Mtendaji

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa Ndg Onesmo Makota amesema kuvunjwa kwa Mamlaka ya mji mdogo na kuanzisha kwa Halmashauri mbili kutasaidia kusogeza karibu huduma kwa wananchi

"Ni sahihi kabisa kuigawa Halmashauri ya Maswa kwa kuwa ni kubwa na Ina majimbo mawili Kata 36, lakini nchi hii Kuna Wilaya Zina Kata 4 au 3 kwa hiyo Kata 36 kuzigakuwa Halmashauri mbili Bado ni sawa, tunasogeza huduma kwa wananchi ili wananchi waweze kufika maeneo ya kupata huduma kwa urahisi."Alisema Mhe. Makota

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe Paul maige alisema lengo la kuwa na mji mdogo ni kusogeza huduma kwa wananchi lakini mapungufu yaliyojitokeza ya dhamira ya kuwa na Mamlaka ya mji

"Mapungufu yaliyojitokeza ikiwa ni pamoja na upungufu wa mapato kwenye eneo la Mamlaka lakini pia na suala la miundombinu kwa sababu hatua hiyo inachelewa kufikia Halmashauri ya mji na Halmashauri ya Wilaya imekuwa na mzigo wa kuendesha Mamlaka ya mji mdogo."alisema Mwenyekiti wa Halmashauri

Ameongeza kuwa ili kuweka tija kwa kuwa na wigo mpana wa kupeleka Fedha za maendeleo  baraza la mji mdogo linapaswa kuvunjwa ili kupata Fedha za kupeleka kwa wananchi kwa ajili ya maendeleo sambamba na hilo kuanzishwa kwa Halmashauri mbili kutusaidia kuwa karibu na wananchi ambapo mchakato ukikamilika utasaidia ongezeko la ajira.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.