Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Dkt Lucy Kulong'wa alisema mafunzo waliyoyapata yakawe chachu ya kutatua changamoto kwa kuhamasisha jamii kuunganisha na kuwa na ushirikiano ili kuleta maendeleo ya jamii nzima katika Kijiji, Kata na Wilaya.
Aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ambayo yalifanyika kwa siku tisa katika makundi tofautitofauti katika shule ya msingi Shanwa.
Mafunzo hayo yaliaandaliwa na mradi wa shule Bora yenye lengo la kuanzisha uhusiano baina ya wazazi na walimu ili kurahisisha shughuli za ujifunzaji hivyo kutoa matokeo chanya kitaaluma na elimu Bora kwa watoto .ambapo wanamafunzo 300 wamepata Elimu ya ushirikiano baina ya wazazi na walimu yaani (UWaWa)
Pia Dkt Kulong'wa alisema kuna changamoto za kimazingira ya kujifunzia ikiwepo uhaba wa madarasa na vyoo hivyo amewataka Walimu Wakuu, Maafisa Elimu Kata na Wenyeviti wa Kamati za Shule kuhamasisha jamii kwa kuwa wamepata mafunzo na miongozo ambayo itawawezesha kutekeleza majukumu yao.
"Mimi naomba nisisitize mkatengeneze mazingira mazuri kwa ajili ya watoto wetu Kuna mambo ya KKK na wanafunzi Wanashindwa kujifunza kusoma na kuandika kutokana na ule mlundikano wa wanafunzi wanakuwa wengi lakini madarasa ni machache naomba haya tuliyoyapata tukayafanyie kazi sisi tutakuja kwa ajili ya ufuatiliaji ili tuone je! Kile mlichojifunza hapa mmekifanyia kazi?"
Aidha aliwataka Wenyeviti kuwapa ushirikiano walimu kwa kuwa Wana jukumu la kulea watoto shuleni hivyo ameiomba jamii kuwathamini Walimu na ameitaka jamii kuepuka migogoro badala yake kuwe na upendo baina ya walimu na wanafunzi ili waweze kufanya kazi yao vizuri.
Kwa upande wake Afisa Mradi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambaye pia ni Afisa Elimu Taaluma Msingi Ndg Neema Makundi alisema mafunzo hayo yalihusisha ushikikishwaji wa mzazi na mwalimu tendo la mtoto kujifunza linahitaji uwepo ushirikiano wa mzazi na walimu, mahusiano mazuri ili kufanikisha tendo zima la utoaji wa Elimu.
Pia Ndg Makundi alisisitita kuwa mafunzo hayo yalilenga kuanzisha uhusiano baina ya wazazi na walimu ili kutoa Elimu iliyo Bora kwa watoto wetu na kwa manufaa ya watoto, Kata na Wilaya.
Nae mwenyekiti wa kamati ya shule kutoka Badi Ndg Andrea Kapene aliishukuru serikali kwa kuwaletea mafunzo hayo kwa kuwa amejua kuwa shule ni mali ya jamii hivyo itakuwa chachu ya maendeleo katika jamii na ameomba mafunzo hayo yaendelee kutolewa zaidi kwa kuwa yatasaidia kuleta faida kwa wazazi.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.