Mafunzo ya Sensa ya watu na makazi ngazi ya wilaya awamu ya tatu yanaendelea kufanyika wilayani Maswa yanayohusisha makarani wa sensa, wasimamizi wa maudhui na TEHAMA ili kupata uelewa wa namna ya kwenda kufanya zoezi la sensa. Mafunzo haya yanaendeshwa katika vituo vitano Wilayani hapa.
Akizungumza katika kituo Cha Binza sekondari Mratibu wa Sensa ya watu na makazi wilaya Ndg; Ntobi Lufunga Ntambi amesema zoezi hili ni muhimu sana katika Taifa hivyo amewaomba wana mafunzo wote waliofuzu saili na kupata nafasi hizo kuwa makini kusikiliza maelekezo yote watakayofundishwa na wakufunzi.
Aidha amewaomba wanamafunzo wote kuwa na nidhamu wakati wa mafunzo kwa sababu kutakuwa na mitihani ambayo itawapima watu wote na kusisitiza kuwa matumizi ya simu hayaruhusiwi katika vipindi vyote wakati wa mafunzo.
Pia mafunzo haya yamejumuisha Watendaji wa Kata ambao walipata elimu hiyo siku mbili za mwanzo ili waende kuhamasisha wananchi kutoa ushirikiano kwa makarani wa Sensa watakaopita Kila kaya kuchukua taarifa zao katika zoezi hilo usiku wa siku ya Jumatatu 22 kuamkia siku ya Jumanne tarehe 23, Agosti 2022.
Kwa upande wake Afisa kutoka Ofisi ya Takwimu amesema Maswa ndio kitovu Cha Mkoa hivyo amewaomba makarani, wasimamizi wa maudhui na TEHAMA kujituma na kuelewa vizuri mafunzo ili waweze kufanya zoezi hilo kwa ufanisi mkubwa na kuubeba Mkoa huu kwa kuwa walimu wako vizuri sana.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.