• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MAFANIKIO YA MUUNGANO KATIKA SEKTA MBALIMBALI WILAYANI MASWA

Posted on: April 29th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amesema serikali ya Wilaya kwa kushirikiana na wananchi imepata mafanikio mengi ambayo inajivunia nayo kutokana na jitihada kubwa zilizofanywa na serikali za awamu ya kwanza, pili, tatu, nne tano na ya sita

Kwa kutoa mchango mkubwa ambapo wananchi walishiriki kikamilifu kuunga mkono jitihada zilizofanywa na waasisi wa Muungano wa Tanzania.  Mkuu wa Wilaya amesema

"Kuwepo kwa Muungano huu ni kuwepo kwa mahusiano ya karibu na ya kihistoria baina ya Tanganyika na Zanzibar katika nyanja mbalimbali kama vile udugu wa damu, biashara, utamaduni, lugha na mahusiano ya karibu kisiasa hususani vyama vya TANU na ASP."

Mkuu wa Wilaya amesema hayo katika kongamano la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania lililofanyika katika ukumbi wa HalmashaurI ya Wilaya ya Maswa Tarehe 26 April 2024.

Mhe Kaminyoge amebainisha kuwa wadau wa maendeleo waliopo ndani na nje ya Wilaya zikiwemo Asasi mbalimbali (madhehebu ya dini, mashirika yasiyo ya kiserikali wamechangia katika sekta mbalimbali za uzalishaji mali, huduma za kijamii utawala Bora na ulinzi na usalama ili kuongeza tija na kuleta mafanikio.

Mkuu wa Wilaya amesema serikali imeendelea kuboresha sekta ya Elimu kwa kutoa Elimu bila malipo ambapo bilioni 2.8 hutolewa Kila mwaka kwa ajili ya Elimu msingi na Elimu Sekondari ikiwa Elimu msingi inapata shs bilioni 1.2 na Elimu Sekondari inapata shs bilioni 1.6

Pia shule za msingi zimeongezeka kutoka shule 27 mwaka 1964 mpaka kufika shule 135 za serikali na binafsi 3 vivyo hivyo Elimu Sekondari haikuwa na shule ya Sekondari na kidato Cha sita lakini Sasa Kuna shule 44 za serikali na 2 za binafsi na shule za kidacho Cha sita 3

Huduma ya afya pia zimeboreshwa sana ambapo vituo vya kutolea huduma za Afya vimeendelea kujengwa na kukamilishwa pamoja na vilivyojengwa kwa nguvu ya wananchi ambapo katika wilaya ya Maswa jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya 56, Hospitali 1, Vituo vya Afya 4 Zahanati 48 za serikali na Zahanati 3 za binafsi

Lengo la serikali ni kuhakikisha huduma hizo zinasogea karibu na wananchi ambapo serikali imeendelea kutoa Fedha zaidi yailioni 600 kwa ajili ya vifaa tiba na dawa ili wananchi wasipate shida.

 Katika sekta ya barabara Wilaya ya Maswa  imeendelea kupiga hatua kubwa kwa kufungua barabara ambapo jumla ya kilometa 1084.2 zinapitika ikiwa lami kilometa 4.78, changarawe 499.27 na udongo kilometa 580.15.

Katika mwaka  wa Fedha 2022/2024 Wilaya ya Maswa imeendelea kuimalisha miundombinu ya barabara, madaraja na vivuko vyenye thamani ya shs bilioni 4 na pia Mhe Rais ametoa shs milioni 100 kwa ajili ya kuirudisha miundombinu ya barabara iliyoharibika katika kipindi Cha mvua jumla ya km 16 za mjini, Lalago na Malampaka kufanyiwa malekebisho.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.