• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Madiwani watakiwa kuanzisha vyanzo vipya vya mapato katika Kata zao

Posted on: September 7th, 2023

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Usimamizi Ufatiliaji na Ukaguzi kutoka Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Ndg. Pius Ngaiza amewataka Waheshimiwa Madiwani kusimamia ukusanyaji wa mapato kikamilifu kwa kuanzisha vyanzo vipya vya mapato vya kisasa na kuachana na vyanzo vidogovidogo ambavyo vinakuwa kero kwa wananchi, na kusimamia maagizo mbalimbali yanayotolewa na serikali ili yatekelezwe kwa wakati.

Pia ameongeza kuwa Waheshimiwa Madiwani  kusimamia ukamilishaji wa miradi ambayo ipo kwa muda mrefu kwa kuongeza kasi katika ukamilishaji wa miradi hiyo kwa kushirikiana na wanachi katika miradi ambayo wananchi wameianzisha ili kuondoa ugumu wa wananchi kuchangia nguvu kazi katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Ameongeza kuwa Waheshimiwa Madiwani wanatakiwa kutoa ushirikiano kwa viongozi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI watakaokuja katika maeneo yao kwa ajili ya kuhakiki maeneo ya Utawala ili  kuandaa utekelezaji wa uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika 2024 hivyo amewataka madiwani kutoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi hao.

Amezungumza hayo katika kikao cha baraza la madiwani cha robo ya nne ya mwaka wa Fedha 2022/2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Leo tarehe 07/09/2023 wakati  wa uwasilishaji wa taarifa za kata katika  kipindi cha robo ya nne ya baraza la madiwani.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mr. Maisha Mtipa ametoa wito kwa watendaji wote wa Kata kuboresha taarifa zao zinazohusiana na masuala ya mapato, miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata zao ili  kuleta ushindani katika kila robo ya mwaka ili kuona ufanisi na utendaji kazi wa viongozi hao katika maeneo yao.

Pia Mr Mtipa amesisitiza kuwa katika hali ya chakula ajenda ya afua za lishe iwe ni muhimu katika miezi 3 kwa kufuatilia hali ya utoaji wa chakula katika shule unaendeleaje na ni shule ngapi zinatoa chakula katika Kata hiyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe Paul Maige amewapongeza watendaji wa Kata kwa usimamizi mzuri wa mapato ya Halmashauri katika maeneo yao kwa kuwa yameimalika.

"Watendaji wa Kata Wana nafasi kubwa sana ya kutufanya tufanikiwe kwa kufikia malengo tuliyojiwekea mkizembea tu maana yake ni kwamba mmeiangusha timu ya menejimenti, mmeliangusha baraza la madiwani kwa maana ya menejimenti na waheshimiwa madiwani nyie ndio mmeshika mpini kwa hiyo Simameni imara kwa yale mazuri mliyoyafanya kama kuna sehemu ambayo hamkufanya vizuri basi hakikisheni mianya hiyo mnaiziba ili tuweze kufanikiwa tunapojiwekea malengo tunahitaji tuyafanye."amesema Mhe. Maige.

Kwa upande wao Waheshimiwa Madiwani wamempongeza Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwepo miundombinu ya afya, barabara, Elimu, maji inayotekelezwa katika Kata zao na wameahidi kuendelea kumuunga mkono katika masuala yote ya maendeleo katika maeneo yao.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.