• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Madiwani wapata mafunzo ya Kilimo Bora cha zao la Pamba

Posted on: September 6th, 2023

Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa Ndg Athuman Kalage amesema kikao hicho kimeitishwa lengo likiwa ni kuwawezesha waheshimiwa madiwani kupata Elimu kuhusu masuala ya kisheria na kanuni za kilimo bora cha pamba kwa kuwa wao ndio wanakaa na wananchi kwa karibu.

Ameongeza kuwa kikao hicho kilikuwa mahususi kwa ajili ya waheshimiwa madiwani ili kuwe na uelewa wa pamoja katika kutekeleza masuala ya Kilimo cha pamba ambacho kitasaidia kuongeza ubora zaidi kuliko sasa.

Aliyasema hayo katika mafunzo ya Kilimo Bora cha zao la pamba kwa waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambapo kikao hicho kilihusisha wakuu wa Divisheni, Kamati ya ulinzi na usalama  na wadau wengine wa masuala ya pamba, balozi wa pamba Tanzania pamoja na viongozi kutoka bodi ya pamba Tanzania.

Mkaguzi wa pamba kutoka bodi ya pamba Tanzania Mr Daniel Bariyanka alisema bodi ya pamba Tanzania imepanga kuanzisha mashamba darasa katika kila Kitongoji  kilichopo katika Kijiji husika lengo ni kuwawezesha wananchi kujifunza kulima kwa kufuata kanuni bora za kilimo cha pamba  kabla ya msimu kuanza ili wakienda kulima waweze kufuata hatua zote zinazostahili ikiwepo kipimo cha sentimita 60 kwa 30 ili walime kwa tija na kupata mavuno mengi.

"Vile vipando sasa tunavitoa Nyakabindi tunataka tuvipeleke katika kila Kitongoji kinachopatikana katika kila Kijiji kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, kama Kijiji kitakuwa na vitongoji 5 kila Kitongoji kitakuwa na kipando kutokana na idadi ya vitongoji vilivyopo katika Kijiji husika". alisema Mr. Bariyanka

Kwa upande wake balozi wa pamba Tanzania Mhe Agrrey Mwanri amewataka madiwani kutoa muda wao kwa kuhamasisha wananchi kuhusu Kilimo Bora cha zao hilo kwa kulipa umuhimu suala hili kwa kuwa waheshimiwa madiwani wamebeba nafasi kubwa katika jamii hivyo wanawajibu wa kusimamia kikamilifu ili wananchi wao waongeze tija na uzalishaji katika zao hilo.

Mashamba darasa hayo yatawekwa katika maeneo ya wazi ambayo yatafikiwa na kila mtu kwa ajili ya kupata ujuzi wa mbinu bora za kilimo cha pamba maeneo hayo yatakoyotumika katika kuanzisha vipando hivyo yatakuwa ni maeneo ya msikitini, kanisani, barabarani, maeneo ya senta, mashuleni, madukani, mashineni ambapo watu wengi wanapita lengo ni kila mkulima aone kwa macho vipimo vya sentimita 60 kwa 30 vinatumikaje shambani.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Maswa Ndg. Makota amewaomba waheshimiwa madiwani na viongozi  kufuata maelekezo ambayo yametolewa kwenye  semina hiyo yakifanyika mara kwa mara wakulima  watabadili mtazamo wa kuweka tija kwenye zao la pamba pamoja na hilo amewaomba waheshimiwa madiwani elimu waliyoipata wakaitumie vizuri kuwahamasisha wananchi wakaone tija inayopatikana baada ya kufuata sheria na kanuni za kilimo hicho.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe Paul Maige amemshukuru balozi wa pamba kwa ushauri aliotoa  kwa kuwa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndio msingi wa mambo yote hayo ya kuongeza uzalishaji kwa kutoka kwenye vipimo vya sentimita 90 kwa 40 kwenda kwenye vipimo vya sentimita 60 kwa 30 ambayo itakuwa imekidhi viwango na kuongeza tija kwa wakulima.

Nae mkuu wa Divisheni ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Ndg. Robert Urassa alisema katika msimu wa 2023/2024 Idara ya Kilimo ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa inatarajia kulima heka 60,438 za pamba na kutalajia kuzalishaji zao hilo kwa wastani wa kg 400 kwa ekari ambapo inatakiwa kuzalisha Tani 60,438.

Pia Mr Urassa ameongeza kuwa mikakati mbalimbali imewekwa ikiwepo kuhamasisha wakulima na viongozi wote juu ya uongezaji tija kwa kufuata kanuni za Kilimo bora cha pamba, kusimamia upatikanaji na ugawaji wa pembejeo za pamba kwa wakati ili kuwasaidia wakulima kulima mapema zao hilo.

Kwa upande wake mkaguzi wa pamba Wilaya ya Maswa Mr Ally Mabrouk alisisitiza ushirikiano kwa viongozi wote katika kuhamasisha wananchi kufuata kanuni 10 za Kilimo cha pamba ambacho kinaanzia hatua ya usafishaji wa mashamba mpaka namna bora ya kuvuna pamba ili kuwasaidia wananchi kupata mavuno mengi katika zao hilo.

Pia ameongeza kuwa wananchi wakitumia kanuni hizo za Kilimo cha pamba watanufaika katika uzalishaji kwa kuongeza tija katika zao hilo ambalo litawaongezea kipato na kuwaletea maendeleo katika uchumi wao.

Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.