• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Madiwani wa Manispaa ya Moshi wanufaika na mafunzo Maswa

Posted on: May 26th, 2022

Madiwani wa Manispaa ya Moshi wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Mhe. Stuart Nkinda na Mkurugenzi wa  Manispaa ya Moshi ndg. Rashid Gembe wamefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu yenye lengo la kubadilishana uzoefu na kujifunza namna ambavyo Halmashauri ya Maswa imeweza kumiliki   Kampuni ambayo inaiingizia mapato Halmashauri.

Waheshimiwa madiwani wa manispaa hiyo wameambatana  na Mstahiki Meya wa Manispaa, Mkurugenzi wa Manispaa, na baadhi ya wataalamu kutoka Manispaa hiyo ya Moshi leo tarehe 26 May 2022.

Wakiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa waheshimiwa madiwani, Mstahiki Meya, Mkurugenzi na wataalamu kutoka Manispaa ya Moshi wametembelea viwanda mbalimbali vya Kampuni ya Ng'hami ambavyo ni Kiwanda Cha Unga wa  Viazi lishe kilichopo Kata ya isanga Kijiji cha Njiapanda, Duka la dawa lililopo Kata ya Sola Kitongoji cha Mwashigela, Kiwanda cha Ngozi kilichopo Kata ya Binza Kitongoji cha Ujenzi, Kiwanda cha kupanga madaraja ya Mchele Kata ya Malampaka Kijiji cha Malampaka, Kiwanda cha Chaki na vifungashio kilichopo Kata ya Nyalikungu Kijiji cha Ng'hami na Kiwanda kinachomilikiwa na kikundi jumushi cha Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu Kiwanda cha Mikate kilichopo Kata ya Nyalikungu Kijiji cha Ng'hami kuona jinsi uzalishaji unavyofanyika

"Nawapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na kuwashukuru watendaji wote wa Kampuni kwa project mbalimbali wanazozifanya Miradi ya ngazi ndogo, ya kati na ngazi kubwa kabisa ni jambo zuri kwa sababu hata kwenye maisha tuna maendeleo kwa ngazi tofauti tofauti kwa hiyo tutaweza kuanza " amesema Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi.

Naye Mkurugenzi  mkuu wa Kampuni ya Ng'hami Ndg. Levocatus Bunduki amewasihi waheshimiwa Madiwani pamoja na Mkurugenzi na wataalamu kutoka Manispaa ya Moshi wanapotaka kuanzisha Kampuni ni lazima wachague mtu amabaye ni mwaminifu na anayejitoa katika kazi yake kwa usimamizi ili Kampuni hiyo iweze kuendelea.

"Mkurugenzi, Mstahiki Meya mnapochagua watu kule chagua mtu mwenye "DNA" ya kuangalia malifedha na malivitu" Bunduki amesema.

Nae  Ndg. Magembe meneja uzalishaji wa Kampuni ya Ng'hami amesema kuwa Kampuni hiyo ilianza mwaka 2019 na mpaka sasa inazalisha bidhaa mbalimbali ikiwepo  Unga wa viazi lishe wa aina mbalimbali , Mchele , pamoja na kutoa huduma ya dawa kwa wahitaji na  mpaka sasa kampuni ina watumishi 17 walioajaliwa,vibarua 22 wa mikataba ya muda mfupi ambao wanafanya kazi katika maeneo tofauti tofauti ya viwanda kwa ajili ya kuongeza thamani na ushindani katika biashara.

Nae Afisa mipango daraja la pili Ndg. Ntobi Ntambi kutoka Ofisi ya  Mipango Wilaya ya Maswa amesema Kampuni imejipanga vizuri kwa kuwa kampuni ilipata fedha bilioni 8.2 zilizotolewa kwenye bajeti ya mwaka 2018/2019 kwa ajili ya viwanda viwili vya Chaki na Vifungashio ambapo mpaka sasa mitambo inaendelea kufungwa katika Kiwanda cha Chaki ambacho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kuzalisha katoni 90 kwa siku za Chaki. Pia kampuni imeweza kutoa gawio la shs milioni 10 kwa wanahisa.




Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.