• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Maadhimisho ya juma la Elimu ya watu wazima yafana Maswa

Posted on: September 25th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mkoa wa Simiyu Mhe Aswege Kaminyoge amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa kwa watoto waliopata ujauzito kupata elimu kama wanafunzi wengine lengo likiwa ni kuwasaidia watoto  wa kike kuendelea na masomo ili watimize ndoto zao.

"Nimpongeze kwa kile alichokieleza kwamba watoto wa kike ambao wanakosa Elimu kwa kupata ujauzito wakishajifungua warudi darasani ili waendelee na utaratibu wa kupata Elimu kama wanafunzi wengine" Amesema Mhe Kaminyoge.

Amesema hayo wakati wa maadhimisho ya wiki ya Elimu ya watu wazima yaliyofanyika katika uwanja wa nguzo nane wilayani Maswa leo tarehe 25.09.2023 wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Dkt Yahaya Nawanda ambapo maadhimisho hayo yamefanyika Kimkoa wilayani Maswa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa, wakuu wa Wilaya za Simiyu, wakurugenzi wa Halmashauri, makatibu Tawala wa Wilaya, maafisa Elimu wakuu wa Divisheni na vitengo walimu pamoja na wanafunzi.

Pia ametoa wito kwa wananchi wote kuwaruhusu wasichana wote waliokatisha masomo wenye sifa za kurudi shule waweze kurejea shuleni na kuendelea na masomo na sambamba na hilo amewataka makatibu tawala wa wilaya zote kuchukua hatua za kisheria kwa watoto wote wanaopata ujauzito  ili watoto hao baada ya kujifugua waweze kuendelea na masomo.

Mhe kaminyoge amewasisitiza wakurugenzi wote kuanzisha madarasa ya kisomo ambayo yatakuwa endelevu ili kukabiliana na tatizo la stadi za kujifunzia yaani kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK)  pamoja na kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuendesha elimu ya watu wazima.

Aidha  amewataka walimu wote waliohitimu stashahada ya elimu ya watu wazima kufundisha na kusimamia elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi katika vituo vyote na shule zenye mahitaji maalumu.

Nae Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu Ndg Majuto Nganja amesema maadhimisho hayo yanalenga kutathmini shughuli za elimu ya watu wazima inavyoendeshwa katika Mkoa wa Simiyu kwa kupata taarifa za utekelezaji wa shughuli za  elimu ya watu wazima kwa kuonyesha shughuli mbalimbali zinazofanyika katika elimu hiyo.

Aidha ameongeza kuwa serikali kupitia mpango wa elimu ya sekondari ulitoa fursa kwa wanafunzi wote walioacha shule kwa sababu mbalimbali ikiwepo ujauzito na mazingira magumu waweza kujiunga na vituo vya elimu ya watu wazima vilivyopo katika Mkoa wa Simiyu.

Pia amesisitiza kuwa wananchi wote ambao  walikosa kusoma  kwenye  mfumo rasmi wanatakiwa kujiunga katika vituo ambavyo vipo katika kila shule ya sekondari na shule ya msingi ili waweze kupata uelewa wa kujua kusoma na Kuandika fursa ambayo italeta maendeleo kwa jamii na nchi nzima kwa ujumla.

Kwa upande wao wasichana wanaosoma katika chuo cha Maendeleo ya Wananchi Malampaka ambao walipata ujauzito wakati wakisoma wamemshukuru Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fursa ya kusoma tena ili waweza kutimiza ndoto zao.  

Kwa upande wake Afisa Elimu ya watu wazima, Elimu nje ya mfumo usio rasmi na Elimu maalumu Mkoa wa Simiyu Ndg Esta Warwa amesema katika Mkoa wa Simiyu vituo 8 vya Elimu mbadala vimeanzishwa kwa ajili ya wasichana waliokatiza masomo ambapo mpaka sasa wasichana 222 wamerudi shuleni kuendelea na masomo na vituo hivyo vipo katika wilaya zote za Simiyu.

Maadhimisho ya juma la Elimu ya watu wazima yamefanyika kwa mgeni rasmi kutembelea mabanda mbalimbali kutoka katika vyuo vya VETA, Vikundi mbalimbali na Banda la stadi za kujifunzia. Maadhimisho hayo kwa mwaka huu yamebeba kauli mbiu ya "Kukuza uwezo wa Kusoma na Kuandika kwa Ulimwengu Unaobadilika: Kujenga Misingi ya Jamii Endelevu na yenye Amani".


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.