• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KUU Wilayani Maswa yakagua miladi ya maendeleo

Posted on: November 19th, 2019

Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Maswa ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hii Mhe. Dr. Seif Shekalage imetembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa hapa ikiwemo na miradi ya kimkakati. Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa ni kama ifutavyo:-


Ukarabati wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa

Katika mradi huu wanakarabati Mabweni, Madarasa, Nyumba 17 za Walimu, Zahanati, Bwalo na Ofisi. Ukarabati huo uko katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo baadhi ya majengo yameishakamilika. Katika ukaguzi huo Mkuu wa Wilaya ametoa maelekezo mbalimbali kwa ajili ya kuboresha shughuli hiyo katika maeneo yote aliyopita na kukagua.

Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani Maswa ikikagua Bweli lililokamilika ukarabati wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo 

Mkuu wa Wilaya ya Maswa akitoa maelekezo kuhusu ukarabati sehemu ya jiko 


Mradi wa Maji Nguliguli

Mradi huu unatarajia kuhudumia vijiji viwili. Katika kijiji cha Nguliguli litajengwa Tenki lenye ujazo wa lita 100,000, Vituo 12 vya kuchotea maji na nywesheo la mifugo 1. Kijiji cha Mwamanenge litajengwa Tenki lenye ujazo wa lita 90,000, Vituo 9 vya kuchotea maji na nywesheo la mifugo 1.

Mkuu wa Wilaya ameagiza Mkandarasi afike eneo la kazi na kuanza utekelezaji wa ujenzi mapema. Aidha ameagiza mkandarasi awasilishe mpango kazi wake wa kutekeleza shughuli hii ofisini kwa mkuu wa Wilaya siku ya Ijumaa.


Miradi ya kimkakati

Inahusisha ujenzi wa Kiwanda cha Chaki na Kiwanda cha Vifungashio katika kijiji cha Ng'hami.  Kakita miradi hii Mkuu wa Wilaya ameagiza taratibu za vifaa vya ujenzi zikamilike haraka na kazi ya ujenzi iendelee.


Ujenzi Ofisi ya Udhibiti Ubora

Ujenzi wa ofisi hii umekamilika, fundi ameahidi kukabidhi jengo kesho, huku samani akisema atakabidhi siku ya Jumapili ya tarehe 24/11/2019.

Kutokana na salio lililobaki Mkuu wa Wilaya ameelekeza wajenge uzio.


Ujenzi wa Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya Maswa

Ujenzi huu uko katika hatua ya ukamilishaji, kazi zilizobaki ni kuweka Vigae, Skiming, Milango na Madirisha. Mkandarasi ameahidi kukabidhi jengo hilo tarehe 15/12/2019.


Mradi wa Maji Mhida

Ujenzi wa Tenki unaendelea na kuweka mtandao wa bomba.

Mkuu wa Wilaya amemuagiza Meneja RUWASA kupeleka mpango kazi wa utekelezaji wa mradi huo.


Mradi wa ujenzi Chuo cha Maendeleo Malampaka

Mradi huu unahusisha ujenzi wa Mabweni 2 na Bwalo, Ukarabati wa vyumba 4 vya madarasa, vyoo, karakana ya ushonaji, maabara ya ICT, Kuchimba kisima na uwekaji wa mfumo wa maji na umeme.

Mhandisi kutoka Wizara ya Elimu baada ya kufanya ukaguzi wa Mradi amesifu jitihada zinazoendelea kwa kazi nzuri na iko hatua nzuri na ameahidi kuongeza nguvu kwenye ukarabati wa Jengo la Utawala.

Aidha kupitia maongezi kati ya Mtaalamu wa Wizarani na Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya ameshukuru kwa utaratibu huo wa Wizara kufika kuona maendeleo ya Miradi yao na kuiomba kuongeza muda zaidi ili kupitia miradi yote.

Kwa msisitizo Mkuu wa Wilaya amewaambia Wahandisi wahakikishe wanafika kukagua na kutoa maelekezo ya kitaalamu kila wiki kwenye miradi hii inayoendelea ili kuwa na majengo bora japo wa majengo mengi ya kusimamia.


Ujenzi wa Kituo cha Afya Mwabayanda

Kazi ya Ujenzi wa Jengo la Wodi ya Wazazi, Upasuaji, Maabara, kuhifadhi maiti na nyumba ya Mtumishi uko katika hatua ya ukamilishaji. Viongozi wamesema imefika muda sasa ujenzi huu ukamilike na majengo yaanze kufanya kazi. Mhandisi amesema Mwezi ujao yatakuwa tayari ya mekamilika.


Shule ya Msingi Mwandu

Katika shule hii vyumba 3 vya madarasa na ofisi viliezuliwa na upepo siku ya tarehe 17/11/2019

Mkuu wa Wilaya amemuagiza Mkurugenzi kuhakikisha ukarabati unafanyika haraka ili kunusuru vifaa vilivyobaki salama na kuweka mazingira ya utayari kwa ajili ya Wanafunzi kuendelea na masomo katika mazingira mazuri ya kujifunzia.

Mkuu wa Wilaya akitoa maelekezo ya kukarabati Jengo lililoezuliwa na upepo katika shule ya Msingi Mwandu



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.