• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kituo cha Zana za Kilimo kunufaisha wakazi wa Maswa

Posted on: February 27th, 2023

Kituo cha zana za kilimo na teknolojia vijijini (CAMARTEC) ni kitovu cha teknolojia ya kihandisi  vijijini taasisi hiyo ipo chini ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Katika Wilaya ya Maswa taasisi hiyo imeanzisha kituo na kitovu cha Teknolojia za kihandisi katika kijiji cha Mwandete Kata ya Sangamwalugesha.

Kituo hicho kinatoa huduma za mafunzo ya teknolojia mpya katika zana za kilimo, matumizi ya gesi itokanayo na vinyesi vya wanyama ( BIOGAS), uuzaji, ukodishaji, matengenezo ya zana hizo na kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu matumizi ya zana na teknolojia hizo kwa wakulima wote wa  Wilaya ya Maswa na nje ya Maswa.

Zana zinazopatikana katika kituo hicho ni Trekta zilizoundwa na taasisi hiyo, Matela ya kubebea mizigo yanayokokotwa na wanyama (Animal drawn carts), mashine za kupandia mazao mbalimbali kwa kutumia wanyamakazi (Mechanical planters), vifaa vinavyotumia nishati ya jua kukaushia mbogamboga, viazi, matunda pamoja na vifa vya kuchemshia maji kwa kutumia mionzi ya jua ( Solar dryer and heaters).

Pia kuna mashine za kupura mazao mbalimbali kama mahindi, mtama, karanga, na alizeti ambazo zinatumia mafuta, (Threshing mashine), mashine za kutengeneza siagi ya karanga (Peanut butter mashine), mashine za kukatakata na kufunga nyasi kwa ajili ya chakula cha mifugo (Straw chopper and hay baler mashine).

Aidha kituo hicho kinatoa huduma ya uwekaji wa vifaa vya gesi asilia  itokanayo na vinyesi vya wanyama kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano kupikia  (Biogas plant installation) pamoja na elimu kwa wakulima kuhusu matumizi ya zana hizo ili kurahisisha ufanisi wa shughuli za uzalishaji.

Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imetoa wito kwa wananchi wote kufika katika kituo hicho ili kujipatia zana, ushauri na kujifunza namna ya kutumia teknolojia mpya ya zana za kilimo.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.