• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kilimo cha mkataba cha zao la pamba Wilayani Maswa

Posted on: August 24th, 2017

Waheshimiwa Madiwani Wilayani Maswa leo tarehe 24/8/2017 wamepewa semina kuhusu kilimo cha mkata hasa katika zao la Pamba.

Kilimo cha mkataba kinamaanisha uzalishaji wa mazao unaofanyika kwa wakulima  kuingia makubaliano (mkataba) na wanunuzi wa mazao hayo. Hapo awali kimekuwa kikitumika tangu kuanza kwa kilimo cha pamba (Vyama vya Ushirika) hadi 1994.

Mkataba unaweka masharti ya namna ya kuzalisha  na kuuza mazao hayo na kila upande huwa na majukumu ya kutekeleza.

Vipengele 3 muhimu vya mkataba:-

i) Upatikanaji wa soko

Mnunuzi na mkulima hukubaliana masharti ya kuuza na kununua zao

ii) Upatikanaji wa pembejeo

Mnunuzi huwa na jukumu la kutoa pembejeo zinazohitajika na wakati mwingine hugharamia kazi ya kuandaa shamba na ushauri wa kitaalam.

iii) Usimamizi Maalum

Mkulima hukubali kufuata taratibu za kitaalam zinazo shauriwa kwa matumizi ya pembejeo,mbinu bora za uzalishaji na uvunaji.

Kilimo kwa njia ya mkataba humlazimisha mnunuzi kujihusisha kwa karibu na uzalishaji wa pamba badala ya kununua na kuondoka.

Faida za kilimo cha mkataba kwa wakulima

i) Kupata pembejeo na huduma za Ugani

  Utaratibu huu utawapa wakulima pembejeo na huduma nyingine kama kuwalimia kwa trakta na huduma za ugani.

ii) Upatikanaji wa mikopo

  Ili kuondokana na tatizo la Wakulima kuwa na pembejeo za kutowatosheleza tunahitaji kutafakari ni jinsi gani mkulima ataongeza tija ambayo itamwezesha kusimamia.

  mradi wake wa kilimo na kuufanya kuwa wa kibiashara.

iii) Matumizi ya Teknolojia Sahihi

 Mbinu mpya za uzalishaji zinahitajika kuongeza kwa hali ya juu ubora wa mazao ya kilimo unaohitajika kwenye soko. Hivyo katika zao la pamba ni lazima huduma za ugani zitolewe baina ya Serikali na wanunuzi wa pamba.

iv) Utoaji wa Ujuzi (Stadi)

 Ujuzi atakaopatiwa mkulima kupitia  kilimo cha mkataba ni pamoja na matumizi sahihi ya viuadudu, matumizi bora ya raslimali,na umuhimu wa ubora wa pamba. Ujuzi na mbinu hizi mkulima huzitumia pia ktk kuzalisha mazao mengine  ya biashara na chakula.

v) Kupata  masoko ya uhakika

Wakulima wadogo wanatatizwa na kukosa fursa ya masoko kwa mazao wanayozalisha hivyo kuwawia vigumu  kubadili na kulima mazao mengine.

Kilimo cha mkataba kinawapa sululuhisho la tatizo hili kwani uwahakikishia soko na kuwapa uhakika wanunuzi wa kupatikana kwa mali ghafi.

Faida ya kilimo cha Mkataba kwa wanunuzi wa pamba

i) Uzalishaji wa kuaminika

 Kilimo cha mkataba ni njia ya kupata malighafi ya uhakika kuliko utaratibu  wa kununua pamba katika masoko ya wazi.

ii) Ubora usiobadilika

 Kilimo cha mkataba kwa kutumia vikundi vya wakulima  kama wakala wa kununua pamba kinalenga kuongeza uwazi ktk magulio na hivyo kupandisha kiwango cha ubora wa pamba.


Aidha wamehimizwa kusimamia suala hili ili utekelezaji wake uweze kuleta ufanisi.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.