• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI YA KUDUMU YA MIKOPO NGAZI YA KATA YAPATA MAFUNZO

Posted on: October 24th, 2024

Kamati ya kudumu ya mikopo ngazi ya Kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imepata mafunzo maalumu kwa ajili ya usimamizi wa mikopo ya asilimia 10 ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

 Mafunzo hayo yametolewa kwa kamati hiyo ambayo inaundwa na Mtendaji wa Kata, Afisa Maendeleo ya jamii, Afisa Ustawi wa Jamii, Afisa Elimu Kata, Maafisa Ugani na Mifugo wa Kata, Watendaji wa Vijiji pamoja na Polisi Kata ili kufahamu kanuni taratibu na miongozo ya utoaji wa mikopo .

Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 23 oktoba 2024 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Awali Serikali ilisitisha utoaji wa fedha za mikopo kwa makundi maalum ya vijana, wanawake na wenye ulemavu kuanzia April hadi Juni, 2023 ili ijipange vizuri kuweka mfumo mpya wa utoaji wa mikopo.

Akifungua mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndugu Vivian Christian amesema serikali imekuja na mpango kazi ambao kila mtu atashirikishwa kwenye ngazi ya eneo husika ili kusimamia kikamilifu utaratibu mzima wa mikopo ya asilimia 10.

Serikali imerejesha rasmi utaratibu wa mikopo isiyo na riba ambayo ilikuwa ikitolewa kwa makundi maalumu ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa lengo la kuwakwamua kiuchumi.

Pia amesema mafunzo kama hayo tayari yametolewa kwa  Kamati ya Ulinzi na Usalama  pamoja na Kamati ya Mikopo ya Halmashauri ya Wilaya.

Aidha ametoa wito kwa washiriki hao kuhakikisha wanasikiliza kwa makini mafunzo hayo ili waweze kutekeleza majukumu yao vizuri kwa kuwa wao ndio watahusika kusaidia nyaraka mbalimbali za wanavikundi ambao wanaishi nao katika maeneo yao.

 Kwa upande wake Afisa maendeleo ya Jamii Lusia Misinzo amesema serikali imeweka utaratibu mzuri ambao umepanua wigo kwa makundi maalum ambapo wanawake, vijana na watu wenye ulemavu wenye umri wa miaka 18- 45 wanaweza kukopa tofauti na awali ambapo serikali iliruhusu  umri usiozidi miaka 35  sambamba na hilo pia mtu binafsi anaweza kukopa lakini lazima awe kwenye kikundi.

 Kamati hiyo itakuwa na majukumu ya kupokea na kuchambua maombi ya mikopo, kufanya tathmini ya awali ya maombi yaliyowasilishwa kwa kutembelea kuhakiki na kushauri vikundi vilivyoomba mikopo na kuandaa taarifa ya hali halisi ya vikundi hivyo na kuwasilisha katika kamati ya mikopo ya Halmashauri.

Aidha kamati hiyo itajikita kwenye ufuatiliaji wa marejesho, kuona maendeleo ya shughuli zao, kushirikisha wadau kutoa mafunzo kwa vikundi na kuwasilisha taarifa ya mikopo kwa kamati ya maendeleo ya Kata.





Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.