• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kamati ya Bunge yaridhishwa na mradi wa uboreshaji usalama wa milki za Ardhi Maswa

Posted on: November 12th, 2023

Kamati ya Bunge, Maliasili na Utalii imefanya ziara katika Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua mradi wa matumizi bora ya milki za ardhi ambao kamati imeridhishwa na mradi huo ambao una faida kubwa ya kusaidia kupunguza migogoro mingi ya ardhi katika mipaka ya vijiji, mashamba na kuboresha usalama wa milki za ardhi kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya ardhi, maliasili na utalii Mhe Timotheo Mzava katika nyakati tofauti walipotembelea na kukagua mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi katika vijiji viwili, Kijiji cha Mwadila kilichopo Kata ya Sukuma na Kijiji cha Igongwa kilichopo Kata ya Ng'wigwa walipokuwa wakigawa hati za kimila 50 kwa kila Kijiji.

"Maelezo tuliyoyapata, maelezo mliyoyatoa nyinyi wenyewe na ramani tuliyoelekezwa sisi kama kamati tumeridhika, kazi hii inafanyika vizuri, tumekuja kuona ni kweli serikali na Wizara wamefanya kazi hiyo vizuri." Amesema Mwenyekiti wa kamati.

Aidha Mhe Mwenyekiti wa kamati amewapongeza wananchi kwa kuupokea mradi huo kwa kuwa utakwenda kuongeza thamani katika ardhi yao na kupitia mradi huo Maisha yao yataboreka.

"Mradi huu ni mradi mkubwa sana unakwenda kuongeza thamani sana lakini kama hauna uthibitisho wa umiliki wa ardhi hiyo wakati mwingine thamani yake inakuwa sio nzuri sana kwa kazi nzuri hii iliyofanywa na Wizara, nataka niwahakikishie kuwa ardhi yenu inaenda kuongeza thamani ". Amesema Mhe Mzava

Pia Mhe Mzava amewasisitiza viongozi wa vijiji kuhakikisha  wanasimamia maeneo yote yaliyotengwa kwa shughuli mbalimbali hayaigiliwi kutokana na makubaliano yaliyo katika mpango huo kwa kuwa serikali imewekeza Fedha nyingi katika mradi huo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Mhe Mbunge Geofrey Pinda  amesema mradi huo una lengo la kufanya maboresho katika vijiji ili kuwe na matumizi bora ya ardhi ambapo mradi huo unatekelezwa katika wilaya saba Tanzania nzima na Maswa ni miongoni mwa Wilaya inayonufaika na mradi huo.

Ameongeza kuwa vijiji 106 vitaandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi ambapo vijiji 5 vitaingia Halmashauri ya mji wa Maswa kwa ajili ya upanuzi  wa mji na vijiji 9 vitapata hadhi ya kuwa miji midogo lengo ni kubeba vijiji vingine ili vikue.

Mpango huo pia utawafaidisha wananchi kwa kuwa hekta  77,666 zimetengwa kwa ajili ya uwekezaji, hekta 481 kwa ajili ya taasisi mbalimbali na hekta 713 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda.

"Nawaomba wananchi kujitokeza kuhakiki majina yenu  ukipata kile kipande cha karatasi unayo haki ya kwenda benki nyie wakulima mnahitaji mikopo masharti yanakuwa mengi lakini ukiwa na hati hii tayari unaweza ukaigia benki na ukaaminiwa ukapewa mkopo kwa sababu wanajua watakukuta wapi." Amesema Naibu Waziri

Nae Afisa Ardhi Wilaya ya Maswa Ndg Vivian Christian amesema mradi huo utasaidia kuthibiti uvamizi katika maeneo yote ya umma yaliyopo katika vijiji hivyo pamoja na kuongeza usalama,ufanisi na suluhisho la utatuzi wa  migogoro kwa wananchi.

Aidha ameongeza kuwa mpaka sasa mradi huo umegharimu shilingi milioni  819 ambapo  vijiji 32 vimeandaliwa mpango wa matumizi ya ardhi   na vipande vya ardhi 19,885 kutoka vijiji 14 vimepimwa na kuingizwa kwenye mfumo na mradi huo utakuwa suluhisho la kuongeza usalama, ufanisi na utatuzi wa migogoro.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.