• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DED Maswa apongeza utekelezaji wa miradi ya BOOST

Posted on: July 29th, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Maisha Mtipa amewapongeza walimu wakuu pamoja na watendaji wa Kata kwa usimamizi mzuri wa miradi ya Boost inayotekelezwa katika maeneo yao.

Ndg. Mtipa alisema hayo wakati wa ziara yake pamoja na baadhi ya wakuu wa Idara walipotembelea miradi hiyo ili kuona hatua ilipofikia na kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ujenzi wa miradi hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji pia amewapongeza mafundi wanaojenga miradi hiyo kwa kuwa kasi yao ni nzuri na pia wanajenga kwa ufanisi na weredi mkubwa pamoja na hilo amewataka waendelee kujenga vizuri kwa kuwa kuna miradi mingi inaendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa sababu Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Elimu ikiwepo SEQUIP.

Akiwa katika ziara hiyo Ndg. Mtipa ametembelea mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu matatu ya vyoo katika shule ya msingi Nguliguli iliyopo Kata ya Nguliguli ambapo mradi huo upo katika hatua ya ukamilishaji na kiasi cha Fedha kilichotumika katika mradi huo ni shilingi milioni 56,000,000/=.

Pia alitembelea Shule ya Msingi Ipililo B iliyopo Kata ya Ipililo ambapo madarasa matatu yamejengwa na matundu matatu ya vyoo mradi huo unaogharimu kiasi cha shilingi milioni 81,300,000/=.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amefika katika ujenzi wa Shule mpya ya Msingi ya mikondo miwili  yenye madarasa 14 ya Shule ya Msingi na Madarasa mawili ya wanafunzi wa awali, matundu ya vyoo 24 na jengo moja la Utawala ambapo mradi huo upo katika hatua ya ukamilishaji na kiasi Cha Fedha kilichotumika katika mradi huo ni shilingi 540, 300,000/=.

Vileve  mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu matatu ya vyoo katika Shule ya Msingi Igunya Kata ya Jija mradi unatekelezwa na serikali kupitia mradi wa Boost ambapo kiasi cha shilingi 56,000,000/= zimetolewa kwa ajili ya kutekeleza mradi huo.

Mkurugenzi Mtendaji pia alitembelea ujenzi wa Shule mpya ya Msingi ya mkondo mmoja katika Kijiji Cha Shishiyu Kata ya Shishiyu wenye madarasa 7 ya shule ya msingi, madarasa 2 ya wanafunzi wa awali na matundu ya vyoo 16 na kiasi cha Fedha kinachotumika katika mradi huo ni shilingi 348,500,000/=.

Pia ziara hiyo ilifika mpaka Kijiji cha Mwakabeya Kata ya Ipililo ambapo ujenzi wa Shule mpya ya Msingi ya mkondo mmoja inajengwa na serikali kupitia mradi wa BOOST kiasi cha shilingi 348,500,000/= zimetolewa ambapo mradi huo unaohusisha ujenzi wa madarasa 7 ya Shule ya Msingi, jengo la Utawala, madarasa mawili ya wanafunzi wa awali na matundu ya vyoo 16.

Halmashauri ya Wilaya ya Maswa inatekeleza miradi hiyo ambayo ilipata Fedha kutoka serikali kupitia mradi wa BOOST kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa shule mpya, madarasa na matundu ya vyoo na mpaka sasa miradi hiyo ipo katika hatua za ukamilishaji.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.