• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MASWA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WATENDAJI WA KATA, VIJIJI NA MAAFISA TARAFA

Posted on: March 6th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge ametoa maagizo kwa watendaji wa Kata, vijiji na Maafisa Tarafa kutatua kero na changamoto za wananchi kwa kufanya mikutano katika maeneo Yao ya kazi.

Mhe Kaminyoge ametoa maagizo hayo katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambacho kimehusisha watendaji wa Kata, vijiji, Maafisa Tarafa na wakuu wa idara.

 Mkuu wa Wilaya amesema hayo ni maelekezo ya  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Dkt Yahaya Nawanda kwa wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji wa Halmashauri ya Wilaya, makatibu Tawala watendaji wa Kata na  watendaji wa vijiji kuhakikisha wanasikiliza na kutatua kero za wananchi katika maeneo Yao.

Mhe. Kaminyoge amesema kuwa ili kutatua kero za wananchi watendaji wa Kata, vijiji na Maafisa Tarafa wanatakiwa kuvua vyeo vyao ili wananchi wafike kwenye ofisi zao ambapo wananchi wanaamini shida zao zitatuliwa.

Pia amewataka watendaji hao kukaa ofisini kwa mujibu wa sheria ambazo ni kanuni za kudumu za utumishi wa umma toleo la mwaka 1999 ambapo mtumishi anatakiwa kuwepo eneo la kazi kuanzia saa moja na nusu mpaka sasa tisa na nusu .

"Mkizingatia haya wananchi wakija wakawakuta kwenye ofisi zenu hatuwezi tukawa na malalamiko kero zingine zitaingia baadae kwa sababu wakati mwingine wananchi wanakuja mara tatu yaani siku tatu ofisi ya Mtendaji wa Kijiji imefungwa , ofisi ya Mtendaji wa Kata imefungwa anaamua kujopa rufaa mwenyewe kuja kwa mkuu wa Wilaya moja kwa moja." Mkuu wa Wilaya

Aidha ametoa maelekezo kwa watendaji wa Kata na vijiji kuanzia kesho waanze kufanya mikutano katika katika maeneo Yao kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi kwa kuzingatia ratiba ya kata husika ili kuniwezesha Mtendaji wa Kata kuhudhuriwa mikutano yote katika vijiji vyake.

Mkuu wa Wilaya ameongeza kuwa Mamlaka ya mji mdogo ipo kisheria hivyo amewataka viongozi wa maeneo hayo wakiwepo wenyeviti wa vitongoji kuhakikisha wanafanya mikutano ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa kutoa majibu ya kero hizo.

Pia Mhe Kaminyoge amewataka  watendaji kuitisha kamati ya maendeleo ya dharura kwa sababu ya kutoa maelekezo kwa wajumbe wote katika Kata kuanzia ngazi ya kitongoji wajue namna ya kutatua changamoto zinazojitokeza katika ngazi hizo kabla ya kufika kwa mtendaji wa Kata.

"Tukifanya hivi Yale malalamiko na kero ambazo zitakuwa zimewashida mzilete na sisi tukaja na kuzitoa kwa njia ya maandishi tuanamaliza kabisa kero mbalimbali zinazowakabili wananchi kero nyingi kwa kweli zipo ndani ya uwezo wetu kwenye maeneo yetu tunayofanyia kazi."Amesema Mhe Kaminyoge


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.