• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC KAMINYOGE AKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA VITUO VYA BINZA NA MALAMPAKA

Posted on: April 25th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge ametoa shukrani kwa Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuboresha sekta ya elimu kwa kuhakikisha miundombinu ya elimu na ufundishaji na ujifunzaji inaboreshwa kwa kutoa vifaa vya tehama vyenye lengo la kuwezesha mafunzo endelevu ya walimu kazini.

Mhe kaminyoge ametoa kauli hiyo wakati akikabidhi vifaa vya Tehama kwa maafisa elimu kata, walimu wakuu vilivyotolewa na serikali kupitia mradi wa BOOST ambapo ametoa wito kwa walimu kuendelea  kufanya kazi kwa bidii, weredi na uadilifu mkubwa  kwa kuwa mpaka sasa matokeo ya elimu msingi na sekondari yamepanda.

“ Maafisa elimu kata na wakuu wa shule hivi vifaa vina gharama kubwa maana yake  vinatakiwa kutunzwa kama mboni ya macho yenu kwa kushirikiana na afisa elimu, uongozi wa serikali ya kata na vijiji vyenu kuhakikisha mnapata walinzi waaminifu ambao watavilinda  na hawatashawishika.” Amesema Mhe. Kaminyoge

Pia Mkuu wa Wilaya amewataka viongozi waliokabidhiwa vifaa hivyo kuhakikisha wanavitunza vizuri na kuviweka kwenye mazingira mazuri yasiyoshawishi kuchukuliwa ili vifaa hivyo vilete tija na kuleta matokeo chanya katika ufaulu.

“Maafisa elimu kata ambao mmepewa jukumu la kuratibu walimu kujifunza kazini hebu pangeni ratiba vizuri ili walimu waweze kupata hayo mafunzo lakini pia afisa elimu ikikupendeza mahali pengine wanapofanya vizuri toa motisha ili na wengine waone.”  Mkuu wa Wilaya

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Vivian Christian amesema wamepokea vifaa hivyo kutoka mkoani vikiwa salama na vitapelekwa kwenye vituo vya Malampaka na Binza kwa ajili ya kujifunzia walimu.

Nae Dkt Lucy Kulon’gwa Mkuu wa Divisheni ya elimu ya awali na msingi Halmashauri ya wilaya ya Maswa ametoa pongezi kwa Mhe Rais kwa kuona umuhimu wa kuleta vifaa ambavyo vitakuwa na umuhimu  mkubwa katika shule hizo.

Amesema vifaa hivyo vitakaa katika vituo hivyo viwili kwa lengo la  kuwawezesha walimu kujifunza na kubadilishana ujuzi katika masomo mbalimbali njia na mbinu za kufundishia ikiwepo mbinu mpya za KKK na pia itasaidia kutumia mitandao ya kijamii kuona namna ambavyo wengine wanavyofundisha ili kurahisisha namna ya ufundishaji.

Aidha Dkt Kulon’gwa ametoa wito kwa walimu kutumia vifaa hivyo na si kuvitunza stoo ili vilete tija kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine ambapo katika kila kituo kinachukua zaidi ya shule 7.

Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imepokea jumla ya kompyuta mpakato 4, Photocopy Mashine 2, projekta 4, Skrini Na Stendi 4, Smart Tv (Inchi 65) 2, Microphone 2, Zoom Kamera 2, Digital Kamera 2 na Wireless Router 2 ambavyo vimetolewa na serikali kupitia mradi wa BOOST kwa ajili ya vituo viwili vya Binza na Malampaka ambavyo vitawezesha utekelezaji wa mafunzo endelevu ya walimu kazini.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.