• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC ayataka Makampuni yanunue pamba kutoka AMCOS

Posted on: July 22nd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amesema makampuni yanatakiwa kununua pamba katika AMCOS kwa sababu pamba hiyo inakuwa na ubora unaotakiwa lengo likiwa ni kupunguza kero ya pamba isiyo na ubora.

Amesisitiza kuwa wadau wa pamba ni wakulima, wanunuzi, AMCOS na serikali hivyo amewataka kuongea lugha moja wanapokutana na changamoto, kero na matatizo katika kipindi Cha ununuzi wa pamba.

Mhe. Kaminyoge ameyasema hayo wakati wa kikao cha wadau wa pamba kutathmini zao la pamba katika ununuzi kwa msimu huu wa Kilimo katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa leo tarehe 22, Julai 2023

 Mhe. Kaminyoge amesema makampuni ya pamba yanatakiwa kutafuta mitaji mikubwa ili kuanzisha viwanda ambavyo vitaongeza thamani kwenye pamba kwa ajili ya  kuwawezesha wakulima kupata soko la uhakika.

Pia amewaomba wadau wa pamba kuendelea kutoa Elimu kwa wakulima kuendelea kuuza pamba yao katika msimu huu pamoja na kuendelea kutoa ufafanuzi kuhusu bei ya pamba kutokupanda kutokana na bei ya soko la Dunia kutokupanda kwa sababu ya nchi nyingi kulima pamba hivyo kusababisha zao hilo lisipande bei msimu huu.

"Bei hiyo ya pamba ni nje ya uwezo wa mkulima, makampuni na ni nje ya uwezo wa serikali, yote haya ni bei ya soko la Dunia, ukilizalisha lazima uliuze na lipate soko likafanye kazi yake, kwa hiyo viongozi mkawaelimishe wakulima waendelee kuuza pamba katika kipindi hiki ambacho serikali inanunua pamba".

Mkuu wa Wilaya amewataka  viongozi wa AMCOS kufanya kazi kwa weredi ili kuleta usawa katika makampuni yanayonunua pamba katika Wilaya yote ya Maswa ili msimu unapofungwa kusiwepo na deni lolote kutoka kwa makampuni au mkulima.

Pia Mhe. Kaminyoge ametoa wito kwa watendaji wa vijiji kusimamia  kwa karibu makampuni yanayonunua pamba katika maeneo kwa kuwa zao hilo linaingizia mapato ambayo inasaidia kuendesha Halmashauri.

Nao wanunuzi wa pamba wameipongeza Wilaya ya Maswa kwa kuwa pamba inayopatikana ni Safi kwa asilimia kubwa haijachanganywa na maji au mchanga hivyo wamewaomba viongozi wa AMCOS kusimamia vizuri pamba na kutenda haki katika ununuzi wa zao hilo.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.