• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC awataka wataalamu kusimamia Kilimo cha Pamba ili wazalishe kwa tija

Posted on: July 16th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amewataka watendaji wa Kata na wataalamu wa Kilimo  kusimamia sheria na kanuni za Kilimo bora cha pamba wanapotoa Elimu hiyo  ili wakulima waweze kulima na kuzalisha  kwa tija kwa kufuata kanuni zote za Kilimo hicho kwa lengo la kuipatia mapato Halmashauri ili iweze kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alisema hayo katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya balozi wa pamba katika kampeni ya kuhamasisha wananchi kufuata kanuni za Kilimo Bora na kutolea maelezo kuhusu bei ya pamba kutokupanda kutokana na wakulima wengi duniani kulima zao hilo, ziara ambayo ilifanyika kwa siku sita katika Wilaya ya Maswa.

Mkuu wa Wilaya alisema serikali inatoa pembejeo pamoja na viuatilifu hivyo watendaji na wataalamu wa Kilimo Wanao wajibu wa kusimamia kikamilifu wananchi kwa kutoa Elimu mapema ya kuandaa mashamba yao baada ya msimu kuisha, hii itasaidia kupunguza changamoto ya wakulima wengi kuacha maotea na kuepuka kuchanganya mazao.

Katika hatua nyingine  Mhe Kaminyoge ametoa wito kwa Mkuu wa Divisheni ya Kilimo mifugo na uvuvi kufuatilia makampuni binafsi yote yanayonunua pamba yaorodheshwe ili kufahamu utaratibu wanaotumia kununua pamba kwa kuwa kuna baadhi ya makampuni yananunua pamba ambayo haina ubora.

Ameagiza kuwa makampuni yote ambayo yatanunua pamba ambayo haina ubora katika wilaya ya Maswa yatafutiwa kibali na hatua kali zitachukuliwa ikiwepo  kupelekwa polisi.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Maisha Mtipa amemshukuru balozi wa pamba kwa kutoa elimu kwa nadharia na vitendo ambayo itawasaidia watumishi watakapofika kwa wakulima kutoa elimu vizuri kuhusu  kanuni bora za Kilimo Cha pamba.

Pia alisema wamejifunza mambo mengi na wamenufaika nayo  ikiwepo ufafanuzi wa bei ya pamba kutokupanda kwa kuwa imewasaidia kwenda kutoa elimu hiyo vizuri endapo watakutana na maswali kutoka kwa wananchi kwa sababu watakuwa na majibu mazuri.

Akitoa taarifa mkuu wa divisheni ya Kilimo, mifugo na uvuvi ndg. Robert Urassa alisema kampeni hiyo imewafikia wananchi 2052 katika vijiji 23 ambao walihudhuria mikutano hiyo ili kupata elimu ya Kilimo Bora cha pamba ambayo imepelekea wananchi 12997 kutoka vijiji 115 kupata elimu hiyo tangu kampeni hiyo ianzishwe mwaka 2021  katika wilaya ya Maswa.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.