• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC atatua kero mbalimbali katika kijiji cha Mwashegeshi

Posted on: October 5th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Mhe Aswege Kaminyoge amefanya ziara katika Kijiji cha Mwashegeshi yenye lengo la kuzungumza na wananchi pamoja na kusikiliza kero na changamoto kwa ajili ya kwenda pamoja katika kutekeleza gurudumu la maendeleo katika Wilaya ya Maswa na taifa kwa ujumla.

Mhe Kaminyoge amesema serikali yoyote duniani imewekwa madarakani na wananchi ili ifanye kazi kwa ajili ya ustawi wa jamii na maendeleo ya kiuchumi kwa niaba ya wananchi.

Amesema hayo leo tarehe 05.10.2023 katika Kijiji cha Mwashegeshi Kata ya Nguliguli wakati akiongea na wanachi hao kwa kusikiliza kero na kutatua changamoto mbalimbali za maji, afya, Elimu na barabara katika kijiji hicho.

Mkuu wa Wilaya amesema jukumu kubwa la serikali iliyopo madarakani ni kuhakikisha wananchi wanakuwa na amani, furaha, utulivu katika kazi zao ili waweze kuzalisha kwa tija katika Kilimo, Mifugo, Biashara pamoja na Uvuvi.

Kwa upande wa maendeleo Mhe Kaminyoge amesema kuwa serikali imetoa Fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miundombinu mbalimbali ya Elimu, Afya, Maji, Kilimo, Mifugo, Barabara na usambazaji wa umeme katika vijiji vyote 120 vya Wilaya ya Maswa.

Ameongeza kuwa Rais ametoa zaidi ya Shilingi milioni 600 kwa ajili ya kupeleka huduma ya maji pamoja na ujenzi wa tenki la maji katika Kijiji hicho ili kuwawezesha wananchi hao wanaotunza chanzo cha maji katika bwawa la zanzui kunufaika na maji hayo.

"Ndio maana Mhe Rais amesema katika  jambo hili nitalifanya kwa nguvu zangu zote ili wananchi wangu wapate maji, ndio maana katika wilaya ya Maswa Sasa tupo katika asilimia 74% kwa wananchi wa vijijini kupata huduma ya maji ndani ya mita 400. Mhe Rais anasema ifikapo 2025 tufikie 85% , lakini kwa mjini tumefikia asilimia 78% tunataka ikifika 2025 wananchi wapate maji kwa 95% majumbani mwao." Amesema mkuu wa Wilaya

Aidha Mkuu wa Wilaya ametoa wito kwa wafugaji kutenga maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo maarufu ngitili ili wapate fursa ya mbegu za majani ambayo yatawasaidia ng'ombe wao kuwa na chakula wakati wa kipindi cha uhaba wa nyasi  kwa kuwa ng'ombe hao watakuwa na chakula cha kutosha hivyo kuwawezesha wafugaji kufuga kwa tija ili kujiongezea kipato kupitia mifugo.

Kupitia  mkutano huo Mhe Kaminyoge amewataka wananchi wote wa Wilaya ya Maswa kuchukua tahadhari katika msimu huu wa mvua ambapo Mamlaka ya Hali ya hewa imetoa utabili kuwa kutakuwa na mvua ya elinino hivyo wanachi wote wanaoishi kwenye mabonde wachukue  tahadhari na popote ambapo uharibifu wa miundombinu utatokea wananchi watoe taarifa haraka iwezekanavyo.

Kwa upande wao wananchi wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea miundombinu hiyo ambayo itawasaidia kupata huduma mbalimbali za kijamii sambamba na hilo wamemshukuru Mhe Mkuu wa Wilaya kwa kufika katika kijiji hicho na kusikiliza kero zao na changamoto zao na wameahidi kuendelea kumuunga mkono katika masuala yote ikiwa ni pamoja na kujitolea nguvu kazi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika Kijiji chao.

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.